Sibuka FM

Baraza la Amani Maswa wafanya kongamano kuliombea taifa, uchaguzi mkuu 2025

20 May 2025, 4:27 pm

Baadhi ya Viongozi wa Dini ya Kiislamu wakiwa katika Dua ya kumuombea Rais Samia na Uchaguzi Mkuu utaofanyika mwezi Oktoba mwaka 2025. Picha na Nicholaus Machunda

Lengo la Kongamano hili la Baraza la Amani ni kuwakutanisha Viongozi mbalimbali wa Dini na kukumbushana nafasi ya Viongozi hao katika kuleta amani hasa kuelekea uchaguzi mkuu utaofanyika mwaka huu pamoja na kuombea Rais Samia anapoongoza taifa kubwa kama Tanzania

Wajumbe wa Baraza  la  Amani  Wilayani  Maswa, mkoani  Simiyu wamefanya Kongamano  la  kumuombea  Rais  wa Jamhuri  ya  Muungano  wa  Tanzania  Mhe  Dkt  Samia  Suluhu  Hassan  pamoja  na  Uchaguzi  Mkuu  utaofanyia  mwezi  Oktoba, 2025

Wajumbe  hao  kutoka  Makundi  mbalimbali  ya  Viongozi  wa  Dini, Wazee  maarufu, Viongozi wa  Kisiasa, Viongozi wa   Tiba  asili na Viongozi  wa  Serikali  lengo  ni  kuhakikisha  amani  ya  Nchi  inadumishwa  hasa  kuelekea  kipindi  ya  Uchaguzi  Mkuu  utakaofanyi  mwishoni  mwa  mwaka  huu  2025

Akimkaribisha  mgeni  rasmi  katika  Kongamano  hilo baada ya  majadiliano ya  ndani,  mwenyekiti  wa  kamati  hiyo  ya  Amani  wilayani  Maswa ambaye pia ni Shekhe wa Wilaya , shekhe    Issa  Elias  amesema  kuwa   yote  waliyokubaliana   wakayaseme  kwa  waumini  wao  huko  Makanisan  na  Misikitini  ili  kila  mmoja  awe  mlinzi  wa  Amani  katika  eneo  lake.

sauti ya Shekhe Issa Elias -mwenyekiti wa kamati ya Aamani- Maswa

Dkt  Vicent  Naano  Anney  ni  Mkuu   wa  Wilaya  ya  Maswa  amesema  suala  la  kulinda  na  utunza  amani ni lamuhimu  sana  hasa  tunapoelekea  kipindi  cha  Uchaguzi  mkuu na  siyo  kuwa sehemu  ya  uvunjivu  wa  amani maana  yapo  mataifa yanatamani  amani tuliyonayo  sisi  Watanzania

picha aliyesimama ni Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt Vicent Anney akizungumza na wajumbe wa baraza la Aamani Maswa
sauti ya Dkt Vicent Anney akizungumza wakati wa Kongamano la amani -Maswa

Aidha  Mhe  Anney  amesisitiza  waandishi  wa  habari  kuwa  na  ueledi  na  Uzalendo  katika  kuandika  habari  na siyo  kila  wakati  kuandika  mabaya  tu  na  Uchonganishi  katika  ya  Serikali  na  Wananchi  wake

sauti ya Dkt Vicent Anney akizungumza wakati wa Kongamano la amani -Maswa

Akitoa  taarifa  kwa  niaba  ya  mwenyekiti,  katibu  wa  Baraza  la  Amani  na  katibu  wa  Bakwata wilayani  hapa,  Maulid  Amir  Mlete amesema  ni  vizuri  kutafakari  kwa  kina kuhusu  Tunu  za  taifa  ambazo  ndio  dira za nguzo na  utulivu  ambao  ziliasisiwa  na  viongozi  wetu  wa  taifa  hili

sauti ya Maulid Mlete – katibu wa baraza la amani Maswa

Kwa  upande  wake  mwenyekiti  wa Parokia  ya  Nyalikungu  wilayani  Maswa  Mwl  Kilama  Mwesiga amesema viongozi  wa  Dini  wanayonafasi  kubwa ya  kuleta  amani na  utulivu  kwa  kuzingatia  Haki  na  Utu  wani  mkiwatendea  haki  wananchi  manung’uniko  na  chuki  zitapungua

sauti ya Mwl Kilama Mwesiga – kutoka Parokia ya Nyalikungu

Onesmo  Makota  ni  Mwenyekiti  wa  chama  cha  Mapinduzi (ccm) Wilayani  hapa  amesema tusikubali  watu  wachache  watushawishi  kuvunja  amani  na  kutufitinisha  kwani  baada  ya  uchaguzi  maisha  yataendelea huku  akisema  ccm  itakuwa  mstari  wa  mbele  katika  kuhakikisha  amani  inatawala.

sauti ya Ndugu Onesmo Makota – Mwenyekiti wa ccm -Maswa
Viongozi wa Dini wakiwa katika Kongamano la Baraza la amani kwa ajili ya kumuombea Rais na Uchaguzi Mkuu mwaka huu
Katibu wa baraza la Amani Maswa akiwasilisha taarifa wa Mgeni rasmi wakati wa kongamano la maombi