Sibuka FM

Hewa tiba yaokoa gharama za matibabu kwa wananchi Simiyu

6 May 2025, 6:17 pm

Muonekano wa mitambo ya kufua hewa tiba(Oksijeni) katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu ambapo inaelezwa na wananchi kuwapunguzia gharama na muda waliokuwa wakitumia kufuata huduma hizo sehemu zingine Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

‘‘Hatuwezi kuwa na taifa lenye uchumi mkubwa kama watu wake wako wanapambana na changamoto ya miundombinu ya afya lazima kwanza tujali afya za watu ambao ndiyo nguvu kazi ya kuyafikia hayo maendeleo ni kweli tumefanya mageuzi makubwa sana katika sekta ya afya sasa kilichobaki ni kuona maendeleo yanaenda kwa kasi ya 5G ili kuyafikia malengo ya viongozi wetu wa kitaifa’’.

Na,Daniel Manyanga

Wakazi wa maeneo mbalimbali mkoani Simiyu wameeleza kuwa uzalishaji wa hewa tiba (Oksijeni) katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu, umewasaidia kuondokana na adha mbalimbali walizokuwa wakizipata kipindi cha nyuma,ikiwemo gharama kubwa za matibabu pindi mgonjwa anapohitaji huduma hiyo ya matibabu ambapo iliwalazimu kufunga safari ya kwenda katika hospitali ya rufaa ya kanda ya Bugando na sehemu zingine.

Kwenye picha ni muonekano wa nje wa jengo mojawapo katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofati na Sibuka Fm,Yohana Isamla, Sabrina Chales na Godfrey Samuel ambao ni wakazi  wa mkoa wa Simiyu wameeleza changamoto walizokuwa wakizipata kabla ya hewa tiba hiyo kuanza kuzalishwa hospitalini hapo.

Sauti ya wananchi wakielezea jinsi ambavyo mitambo hiyo imewapunguzia gharama za kufuata huduma kama hiyo sehemu zingine

 Dk. Juma Muna ni mratibu wa huduma za tiba katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu na hapa anaeleza namna ambavyo uzalishaji huo wa hewa tiba umekuwa msaada kwa wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo  huku mhandisi wa vifaa wa hospitali hiyo, Bathromeo Kapuga akieliza hali ya uzalishaji wa hewa tiba hiyo hospitalini hapo.

Sauti ya wataalamu wa vifaa hivyo wakizungumza namna mitambo hiyo imekuwa msaada mkubwa kwenye matibabu kwa wananchi wanaohitaji huduma hiyo

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Simiyu Kenani Kihongosi, ameeleza namna ambavyo serikali imefanya maboresho ya huduma za afya katika mkoa wa Simiyu katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ambapo ameleta fedha nyingi ambazo zimefanya mageuzi makubwa kwenye sekta ya afya.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Simiyu, Kenani Kihongosi akielezea namna ambavyo serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania alivyoweza kutoa fedha nyingi katika kuboresha miundombinu ya afya mkoani hapo.