Sibuka FM

Maswa yaadhimisha kivingine miaka 61 ya  Muungano wa Tanzania

26 April 2025, 6:40 pm

Picha ni Washiriki wa Bonanza la sherehe za Miaka 61 ya Muungano wa Tanzani wakiwa katika Mazoezi ya viungo katika Uwanja wa ccm nguzo nane Mjini Maswa. Picha na Nicholaus Machunda

Muungano  ni  Tunu  ya  Taifa  hivyo  hatuna  budi  kuulinda  na  kuudumisha   na  kuwapuuza  wale  wachache  wanaoleta  chokochoko  juu  ya  Jamhuri  ya  Muungano  wetu  wa  Tanzania ” DC Maswa Mh Dkt Vicent Naano wakati akifungua Bonanza la Maadhimisho ya sherehe za miaka 61 ya Muungano”

Na Nicholaus Machunda

Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa, Mkoani  Simiyu  imesherekea  kitofauti  miaka  61  ya  Muungano  wa  Tanganyika  na  Zanzibar  na  kuunda  Tanzania   kwa  kufanya  Bonanza  la  Michezo  mbalimbali ikiwemo  Mpira  wa  Miguu,  kuvuta  kamba,  Kukimbia  na Magunia, Kunywa  soda  na  Mkate  Pamoja  na   kucheza  mziki,

Akifungua  bonanza  hilo ,  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Mhe  Dkt  Vicent  Naano  Anney  amesema  kuwa  Muungano  ni  Tunu  ya  Taifa  hivyo  hatuna  budi  kuulinda  na  kuudumisha   na  kuwapuuza  wale  wachache  wanaoleta  chokochoko  juu  ya  Jamhuri  ya  Muungano  wetu  wa  Tanzania

Bonyeza hapa kusikiliza sauti Dc Maswa akifungua bonanza la sherehe za miaka 61 ya Muungano

Mhe  Dkt   Naano  ameongeza  kuwa  ni  vizuri  kuwa  na  mwendelezo  wa  Bonanza  kila  mwisho  wa  Mwezi  ili  Mji  uweze  kuchangamka  huku  akiahidi  kuanzisha  Ligi  yake  itakayoitwa  Samia  Cup  kwa  kushirikisha  makundi mbali mbali  ili  Mji  uchangamke  na  watu  kufanya  biashara  mbalimbali.

Bonyeza hapa kusikiliza sauti Dc Maswa akielekeza kuwa na mwendelezo wa mazoezi na Bonanza
picha ni Burudani ya washiriki wakishindana kunywa soda na Mkate katika Bonanza la miaka 61 ya Muungano

Saidi  John  Mshana  ni  Afisa  Utamaduni  na  Michezo  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  ametaja  Michezo  mbalimbali  iliyofanyika   katika  Bonanza  hilo  la  kusherekea  Miaka   61  ya  Muungano  wa  Tanzania  lililokuwa  limefana  kutokana  na  Ubunifu  wa  Michezo  mbalimbali

Hii hapa sauti ya afisa Michezo akielezea michezo iliypokuwepo katika bonanza hilo

Aidha   Mshana  amesema  kuwa  kutakuwa  na  mwendelezo  wa  Bonanza  kila  mwezi  kama alivyoagiza  Mkuu  wa  Wilaya   kwa  lengo  la  wananchi  kushiriki  kufanya Mazoezi  ili  kujiepusha  ya  Magonjwa  yasiyo  ya  kuambukizwa

Hii hapa sauti ya afisa Michezo akielezea mwendelezo wa mazoezi na Bonanza
Watoto pia hawakusahaulika nao walishiriki mashindano na Michezo mbalimbali

Baadhi  ya  Wananchi  walioshiriki  bonanza  hilo   Wamewashukuru  Viongozi  wa  Wilaya  kwa  Kuandaa  michezo  hiyo  kwani  imewaweka  karibu  pamoja  na  ushirikiano  kati  ya  Wanachi  na  Viongozi  wa  Serikali

Hizi hapa ni baadhi ya sauti za Wananchi walioshiriki mazoezi hayo na Bonanza la sherehe za miaka 61 ya Muungano wa Tanzania

Naye  Kaimu  Mkurugenzi  Mtendaji  wa   Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa   Ndugu  Vivian  Christian  amewashuru   Watumishi, Taasisi  na  Wananchi  kwa  kushiriki  Bonanza  la  sherehe  za  Muungano  huu  akiwaalika  kujitokeza  kwa  Wingi  katika  Sherehe  za  Siku  ya  Wafanyakazi (Mei Mosi )  ambapo  kimkoa  zitafanyika  Wilayani  Maswa

sauti ya Kaimu Mkurugenzi Halmashauri Ndugu Vivian Christin akiwashukuru wote walishiriki bonanza hilo
Picha ni wachezaji wa timu ya Utumishi Combain wakiwa tayari kushiriki bonanza
Picha ni wachezaji wa timu ya Usalama wakijiandaa kwa mchezo wa Mpira wa Miguu