Sibuka FM

Mil.173.6 zatolewa  kwa vikundi vya uzalishaji  mali wilayani Maswa

27 March 2025, 9:28 am

Picha: aliyesimama (ameshika Mic ) ni Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt Vicent Naano Anney akizungumza wakati wa Hafla ya kukabidhi Mikopo kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu, kushoto kwake mwenye Miwani ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Maswa Robert Urassa na kulia kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe, Paul Maige. Picha na Nicholaus Machunda

Lengo  la  Mikopo  hii  ni  kuwakomboa  watanzania   kiuchumi  na  hivyo muwe  waaminifu  katika  Marejesho  ya Mikopo yenu mliyopewa ili  watanzania  wengine  waendelee  kukopa na siyo kwenda kunywea Pombe na kununua Vitenge “Dc Maswa Dkt Vicent Naano “

Zaidi  ya  shilingi  Milioni   173 zimetoewa   na  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa   kwa  Vikundi  15  vya  Uzalishaji  Mali  vya  Wanawake,  Vijana  na    Watu  wenye  Ulemavu   kama  gawio  la  asilimia  10 ya  Mapato  ya  ndani  ya  Halmashauri.

Akizungumza  na  wana  vikundi   waliopokea Mkopo  huo, Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Dkt   Vicent  Naano  Anney  amesema  kuwa   lengo  la  Mikopo  hiyo  ni  kuwakomboa  watanzania   kiuchumi  na  kuwataka   kuwa waaminifu  katika  Marejesho  ili  watanzania  wengine  waendelee  kukopa

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa dkt Vicent Naano

Aidha  Dkt   Vicent  Naano   amemuagiza  Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri   kuhakikisha  wote  waliokopa  na  wakashindwa  kurejesha   wasakwe  na  wakatwe  kisha  wapelekwe  Mahakamani  ili  waweze  kurejesha  fedha  hizo   ili Vikundi  vingine  waendelee  kukopa   na  kujikwamua   Kiuchumi

Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa dkt Vicent Naano

Akitoa  taarifa  kwa  Mgeni   rasmi,  Kaimu  mkuu  wa  Divisheni  ya Maendeleo  ya  Jamii  wilayani  hapa  Bi  Basila  Bruno  amesema  kuwa  jumla  ya  Vikundi   15   vya  Wanawake,  Vijana  na  watu  wenye Ulemavu   vyenye  wananchama  105   wamepatiwa  Mikopo  hiyo  kwa  awamu  ya  kwanza.

Sauti ya Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii wilayani Maswa

Robert  Urassa  ni  Kaimu  Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri  ya  wilaya  ya  Maswa   amesema  kuwa  hategemei  kuona  vikundi  hivyo    mwakani  vinaomba  mikopo  tena  na  badala  yake  mitaji  hiyo  iwasaidie  kuwainua  zaidi  kiuchumi   na  kutoa  marejesho  ili  waendelee  kutoa  mikopo  kwa  vikundi  vingine.

Sauti ya Robert Urassa Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Maswa

Akimwakilisha  Mbunge   wa  Jimbo  la  Maswa  Mashariki  Mhe  Stanstaus  Nyongo,  Marco  Bukwimba  ni  katibu  wa  Mbuge  amewataka  walengwa  waliopata Mikopo   kwenda  kutekeleza  waliyoelekezwa  na  wataalamu  ili  fedha  hizo  ziwanufaishe   na  siyo  kwenda  kulewa  Mvinyo  na  kununua  vitenge

Sauti ya Marco Bukwimba – mwakilishi wa Mbunge Jimbo la Maswa Mashariki

Katika  hafla  hiyo  ya  kukabidhi   Mikopo  kwa   Vikundi  vya  Uzalishaji  mali   vya  Wanawake, Vijana  na Wenye  Ulemavu   imehudhuriwa  na  mwenyekiti  wa  Halmashauri   hiyo  Mhe,   Paul  Maige   na  kuwataka   walengwa  kwenda  kusimamia  malengo  yao ili  fedha  hizo  zilete  matokeo  tarajiwa

Sauti ya Paul Maige Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
Wana Vikundi kutoka maeneo mbalimbali wilayani hapa wakiwa wanasikiliza Maelekezo ya Viongozi (hawapo pichani ) kuhusu Matumizi ya Mikopo yako wakati wa hafla ya kukabidhiwa

Baadhi  ya  walengwa  wa  Vikundi    waliopata   Mikopo  hiyo (Elias Emmanuel  na Zawadi  Pima ) wameishukuru  Serikali ya  Mhe,   Rais  Dkt  Samia  Suluhu  Hasani  kwa  kutoa  mikopo  hiyo  kwani  itaenda  kuwainua   Kiuchumi  huku  wakiahidi   kurejesha   kwa   wakati  ili   vikundi  vingine   waweze   kukopeshwa.