Sibuka FM

IPOSA yatajwa kuwakwamua vijana kiuchumi mkoani Simiyu

19 March 2025, 4:55 pm

Muonekano wa picha ya pamoja ya wanafunzi wakiendelea kupata elimu ya ufundi katika moja wapo ya chuo cha ufundi hapa nchini Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

‘‘Aliyesema kuwa elimu ni ufunguo wa maisha ni kweli hakukosea ndiyo tunawatu wengi sana ambao hawakuweza kupata elimu ndani ya mfumo rasmi lakini haimaanishi kuwa watu hawa wasiweze kupata fursa ya elimu hata ya ufundi stadi ili kuondoa utegemezi kwenye familia zao’’.

Na,Daniel Manyanga

Imeelezwa kuwa utekelezaji wa mradi wa IPOSA ambao una lengo la kuwafikia na kuwanufaisha vijana wenye umri wa miaka 14 – 19 ambao hawakupata fursa ya elimu kupitia mfumo rasmi mkoani Simiyu utakuwa ni mkombozi kwa vijana hao kwani utawawezesha kujikwamua kiuchumi kupitia shughuli mbalimbali watakazokuwa wakizifanya kutokana na mafunzo watakayoyapata kupitia mradi huo.

Vijana wakiwa katika majukumu ya kutekeleza elimu ya ufundi kwa vitendo Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

Hayo yamesema na katibu tawala msaidizi anayeshughulikia masuala ya uchumi na uzalishaji mkoani Simiyu, Juma Topera wakati akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo ,Kenani Kihongosi wakati wa kufunga mafunzo ya siku 21 ya walimu watakaokuwa wakiwafundisha vijana hao fani mbalimbali kupitia mradi huo wa IPOSA, na kueleza namna ambavyo mradi huo ni muhimu kwa vijana wa mkoa wa Simiyu.

Sauti ya katibu tawala msaidizi maswala ya uchumi na uzalishaji akielezea umuhimu wa ujuzi kwa watu ambao wapo nje ya mfumo rasmi na wale ambao wapo kwenye mfumo rasmi wa ajira

Awali akitoa taarifa juu ya mafunzo hayo mkufunzi mkazi kutoka taasisi ya watu wazima mkoa wa Simiyu, Chago Igoloka, amesema kuwa mradi unalenga kuwawezesha vijana hao ili wasiachwe bila msaada wa kielimu huku mhadhiri msaidizi kutoka taasisi ya elimu ya watu wazima, Rose Mgaya akieleza kilichowasukuma kuanzisha mradi huo kwa ajili ya kuwasaidia vijana ambao hawajapata elimu katika mfumo rasmi wa serikali.

Sauti ya watekelezaji wa mradi huo wakizungumzia sababu za kuja mradi kama huo hasa kwa vijana waliokosa elimu katika mfumo rasmi

Alfred Thobias, Mary Manfred na Noel Mlunde ni baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo ya siku 21 wameeleza namna ambavyo yatasaidia kuwakwamua kiuchumi vijana waliolengwa kufikiwa na mradi huo.

Sauti ya walimu watakaoenda kuwafundisha vijana ujuzi mbalimbali wakielezea namna elimu hiyo itakuwa msaada mkubwa kwa vijana