Sibuka FM

Stakabadhi ghalani yarudisha thamani kwa wakulima Maswa

15 February 2025, 12:40 pm

Muonekano wa ghala likiwa tayari kwa kuhifadhia mazao wakati wa msimu wa ununuzi na uuzaji kwa kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

‘‘Kilimo ni moja wapo ya sekta ambayo imeajiri watu wengi sana na nimuhimu sana katika ujenzi wa taifa maana hatuwezi kuwa na uchumi imara wakati watu wake wanalia njaa hiyo siyo ajenda ya taifa lazima wakulima tuwalinde na kuwapa thamani kutokana na kazi kubwa wanayoifanya ya kuzalisha chakula’’.

Na,Daniel Manyanga

Wakulima wa zao la choroko wilayani Maswa mkoani Simiyu wameishukuru serikali mkoani humo kwa kuanzisha mfumo wa stakabadhi ghalani katika uuzaji wa zao hilo mfumo ambao wameeleza kuwa unawanufaisha kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na hapo awali kabla ya matumizi ya mfumo huo kuanza.

Wakizungumza Sibuka fm kwa nyakati tofauti wakulima hao wameeleza manufaa wanayoyapata kwa sasa katika uuzaji wa mazao yao kupitia stakabadhi ghalani kufuatia serikali mkoani hapo kuanza kutumia mfumo huo hali ambayo inalengo la kuwainua wakulima kutokana na kazi kubwa wanaifanya wakati wa msimu wa kilimo.

Wamesema kuwa mwanzoni mkulima alikuwa hapewi thamani kubwa kama leo hii kutokana na mfumo huo wa uuzaji wa zamani kuwaibia wakulima hali ambayo iliwafanya wengine kuangalia namna nyingine ya kuachana na kilimo lakini ujio wa stakabadhi ghalani utawafanya walime kwa tija.

Sauti ya wakulima wakizungumzia manufaa ya stakabadhi ghalani

Kwa upande wake ,Ntemi Mpina ambaye ni mmoja wa wafanyabiashara ya mazao mbalimbali ya nafaka wilayani Maswa  ambayo kwa sasa yanauzwa kwa kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani ameeleza faida za matumizi ya mfumo huo.

Sauti ya mmoja wa wafanyabiashara wa mazao mchanganyiko akielezea namna ambavyo ununuzi na uuzaji wa stakabadhi ghalani utakavyoweza kuwanufaisha na wao