Sibuka FM

Maswa:kesi za mirathi,ardhi na ndoa zatawala wiki ya sheria

4 February 2025, 11:19 am

Picha ya pamoja ikiwaonyesha mkuu wa wilaya ya Maswa, Aswege Kaminyoge mwenye suti akivalia tai ya rangi ya karoti na miwani na hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Maswa,Mhe.Enos Missana wakifuatilia kwa umakini mkubwa jambo linaloendelea Picha na Paul Yohana

‘‘Hivi hatuwezi kumaliza migogoro ya ardhi,mirathi na ndoa kwenye jamii zetu sheria zinasemaje kwa mtu ambaye atafanya kesi za aina kama hiyo kama changamoto ni sheria zetu basi tuziboreshe  na kama ni elimu ndogo ya kisheria kwa wananchi wetu vyombo vinavyohusika kutoa elimu wanajukumu kubwa la kumaliza migogoro hiyo’’.

Na, Paul Yohana

Migogoro ya ardhi,mirathi na ndoa imetajwa ni kesi zinazoongoza kulipotiwa katika mahakama za wilaya ya Maswa mkoani Simiyu  hali ambayo inachangiwa na uelewa mdogo wa maswala ya kisheria kwa wananchi wanaoshtakiana kwenye vyombo vya sheria.

Hayo yamesemwa na hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya Maswa,Mhe.Enos Missana  wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria nchini ambapo kwa  wilaya ya Maswa yamefanyika kwenye viwanja vya mahakama na kuhudhuriwa na wadau wa mahakama.

Missana amesema kuwa kutokana na uchunguzi uliofanywa katika wiki wa sheria wamebaini kuwa asilimia kubwa ya wananchi hawana uelewa wa  maswala ya kisheria hivyo kuchangia migogoro mingi ambayo wakati mwingine ingeweza kumalizikia huko nyumbani bila hata ya kufika katika vyombo vya sheria.

Sauti ya hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Maswa,Mhe.Enos Missana akizungumza na hadhara katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria

Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Maswa,Mhe.Enos  Missana ameongeza  kuwa mahakama itahakikisha elimu hii inaendelea kutolewa hata baada ya maadhimisho ya wiki ya sheria nchini pamoja  kuanzishwa kwa  klabu  mbalimbali na kushirikisha wadua wa mahakama katika kutoa elimu kwa wananchi juu maswala ya kisheria ili kupunguza migogoro  kwa jamii.

Sauti ya Mhe.Enos Missana hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama akielezea mkakati katika kuendelea kutoa elimu ya sheria
Kwenye picha ni muonekano wa hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Maswa,Mhe.Enos Missana akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria Picha na Paul Yohana

Akizungumza  katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria mgeni rasmi ambaye ni  mkuu wa wilaya ya Maswa ,Aswege Kaminyoge amewaomba wananchi kushirikiana na mahakama na vyombo vingine vya dola ili kuhakikisha elimu ya maswala ya kisheria inamfikia kila mwananchi hali ambayo itapunguza migogoro kwenye jamii zetu.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Maswa, Aswege Kaminyoge akitoa wito kwa vyombo vya sheria kuendelea kuwa msitari wa mbele kutoa elimu
Kwenye picha ni muonekano wa mkuu wa wilaya ya Maswa, Aswege Kaminyoge akizungumza jambo katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria nchini Picha na Paul Yohana

Nao  baadhi ya wananchi waliohudhuria maadhimisho  wamesema kuwa elimu ndogo ya kisheria juu ya maswala ya ardhi , mirathi  na ndoa ndiyo imekuwa janga kubwa la mauwaji mbalimbali kwa wananchi yanayotokea  hivyo elimu itolewe bila kuwa na ukomo na hii itasaidia kupunguza migogoro kwenye jamii zetu.

Sauti ya mwananchi akielezea namna ambavyo migogoro ya ardhi inavyoathiri wananchi
Pichani ni mwendesha mashtaka mwandamizi kutoka ofisi ya Taifa ya mashtaka wilaya ya Maswa, Vailet Mshumbusi akizungumza jambo katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria nchini Picha na Paul Yohana