Sibuka FM

Bariadi:Wanandoa waathirika wa Ukimwi wapata mtoto asiye na maambukizi

10 July 2024, 3:59 pm

Pichani ni mratibu wa ukimwi mkoa wa Simiyu Dk.Khamis Kulemba akizungumza wakati wa afua za ukimwi Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

“Kupata ukimwi siyo mwisho wa maisha na wala siyo kiama vijana wawili wilayani Bariadi wa jinsia ya kiume na kike ambao ni waathirika wa ukimwi wamezaa mtoto ambaye hana virusi vya ukimwi’’

Na,Daniel Manyanga

Watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi wilayani Bariadi mkoani Simiyu wameiomba serikali na wadau wa masuala ya afya kuendelea kutekeleza afua za Ukimwi  ambazo hapo awali zilikuwa zikiwakutanisha pamoja na kuwasaidia kujiamini na kuendelea kutumia dawa za kufubaza makali ya virusi hivyo pasipo kukata tamaa.

Akizungumza na  Sibuka Fm mjini Bariadi, James Nyamoye ambaye ni kijana mwenye umri wa miaka 29 anayeishi na virusi vya Ukimwi  alivyozaliwa navyo, ameeleza namna ambavyo kambi zilizokuwa zikiwakuatanisha pamoja zilikuwa zinawasaidia kutokata tamaa kutumia dawa za kufubaza na kuondoa unyanyapaa kwa jamii wanayoishi.

Sauti ya James Nyamoye ambaye ni mwathirika wa ukimwi akizungumza

Mary James ni mke wa James Nyamoye ambaye anaeleza namna alivyoweza kuzingatia maelekezo aliyopewa na wataalam wa afya katika kambi zilizokuwa zikiwakutanisha watu wenye VVU na kumuwezesha kupata watoto wawili ambao hawana maambukizi.

Sauti ya mke wa James akielezea namna alivyoweza kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya

Kwa upande wao ndugu wa watu wenye maambukizi ya VVU wameeleza namna ambavyo makongamano yaliyokuwepo awali ambayo yaliwakutanisha vijana wenye maambukizi kutoka maeneo mbalimbali yalivyowasaidia  kukabiliana na VVU.

Sauti za ndugu

Akitolea ufafanuzi suala la hilo mratibu wa kuthibiti maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na Ukimwi, homa ya Ini pamoja na magonjwa ya ngono mkoa wa Simiyu Dk. Khamis Kulemba ameeleza jitihada zinazofanywa ili kuhakikisha watu wanaoishi na VVU wanapata huduma stahiki.

Sauti ya mratibu wa kuthibiti ukimwi mkoa wa Simiyu Dk.Khamis Kulemba