Sibuka FM

TRA yatoa elimu kwa wafanyabiashara ulipaji kodi kwa hiari

28 May 2024, 5:03 pm

Pichani wa kwanza (mwenye shati ya Njano) Benjamin John Afisa Elimu na Huduma TRA Mkoa wa Simiyu akifuatiwa na Lucius Theonesti Meneja TRA Maswa, katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge na wa Mwisho kwake ni Athumani Kalaghe DAS Maswa Wakati wa Utoaji wa Elimu ya Mlipa Kodi kwa Wafanyabiashara

Wafanyabiashara wilayani Maswa wamepewa elimu ya ulipaji kodi kwa hiari ili kujenga uchumi wa nchi, pia kikao hicho kimehudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Aswege Kaminyoge na maafisa wa TRA kutoka wilayani hapo na mkoa.

Mamlaka  ya  Mapato  Tanzania  TRA  mkoa  wa  Simiyu  imeendesha  mafunzo  kwa  wafanyabiashara  wilayani  Maswa  kuhusu  elimu  ya  kulipa  kodi  kwa  hiari  ili kuleta  huduma  bora  za  jamii na uchumi  wa  taifa

Akifungua  mafunzo  hayo  Mkuu  wa Wilaya  ya  Maswa  Mh.  Aswege  Kaminyoge  amesema  kuwa   utunzaji  wa  kumbukumbu  za  mauzo  ya  bidhaa  ni  muhimu  kwa  mfanyabiashara  pamoja  na  kuwa  na uwazi na  uzalendo  katika  kulipa  kodi  kwa  hiari.

Sauti ya Aswege Kaminyoge – DC Maswa akizungumzia ulipa Kodi

Mh Kaminyoge  amesema  kuwa  lazima  watoe  rist  za  EFDs  wanapofanya  Manunuzi   na  Mauzo  ya  Bidhaa  zao  ili  kuwarahisishia  maafisa  wa  TRA kukadiria  kodi  kulingana  na  Mauzo yanayopatikana  huku akiwataka wafanyabiashara  ambao  hawajafikia kuwa  na  EFDs  watoe  rist  za  Mkono  ili  kuweka  kumbukumbu.

Sauti ya Aswege Kaminyoge – DC Maswa akizungumzia ulipa Kodi

Meneja  wa  TRA  Wilayani  Maswa    Lucius  Theonesti   amesema  kuwa  bado  matumizi  ya  Mashine  za  EFDs  ni  madogo  hivyo  amewataka   wafanyabiashara  watumie  hizo  Mashine kwa  walio  na vigezo ili  kuondoa  malalamiko  ya  kukadiriwa   Kodi  kubwa.

Sauti ya Lucius Theonesti Meneja TRA Maswa Sauti ya Lucius Theonesti Meneja TRA Maswa

Aidha  amesititiza  kwa  Wafanyabiashara  kuwa  waaminifu  na  wazalendo  kwani  wapo  baadhi  yao  wanapotembelewa  na  Maafisa  wa  TRA    Wanaficha  vielelezo  vyao   vya  kumbukumbu  ya  Mauzo  ili  kukwepa  kulipa   Kodi  halali.

Sauti ya Lucius Theonesti Meneja TRA Maswa akielezea ulipaji Kodi kwa Wafanyabiashara

Nao  baadhi  ya  Wafanyabiashara   John  chagu  na   Zainabu  Masoud   wamesema   ni  vyema  ikatumika  Lugha  ya  Kiswahili katika  Nyaraka  za TRA  ili  kumrahisishia  mteja  kuelewa  zaidi   pamoja  na  kuwatembelea  mara  kwa  Mara  ili  kuona  changamoto  zinazowakabiri  ili  kufanya  Makadirio  sahihi.

Sauti ya John Chagu na Zainabu Masoud Wafanyabiashara Maswa
Pichani ni Wafanyabiashara Wilayani Maswa wakisikiliza kwa Makini Elimu ya Ulipaji Kodi kwa Hiari ikitolewa na Maafisa wa TRA (hawapo pichani) katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Chupa kubwa Mjini Maswa.