Sibuka FM

Maswa yatapakaa uchafu, wajumbe wacharuka

26 January 2026, 2:13 pm

Aliyesimama ni Bi Caroline Shayo mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Maswa akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Mamlaka ya Mji kilichofanyika katika ukumbi wa mamlaka maeneo ya Ujenzi mjini Maswa, kushoto kwake ni Bi Veronica Mbiha Mtendaji wa Mamlaka na wa mwisho ni Ndugu Vivian Christian Kaimu DED Halmashauri ya Maswa – Picha na Nicholaus Machunda

Mji wetu wa Maswa ni mkubwa unahitajika usafi wa mara kwa mara, unapoitoa treka site hasa kipindi hiki cha mvua tunaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa yanayotokana na uchafu wa mazingira- “Caroline shayo Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Maswa”

Wajumbe wa  Baraza  la Mamlaka ya Mji mdogo Maswa wamelalamika kukithiri kwa uchafu katika mji  huo kutokana na trekta  linalotumika katika shughuli za kuzoa taka  kubadilishiwa  matumizi hali  inayoweza kusababisha magonjwa ya mlipuko.

Wakichangia  katika  kikao cha baraza la mamlaka cha robo ya kwanza ya mwaka wa  Fedha  2025/2026  wajumbe hao wamesema  kuwa  trekta linalotumika  kuzoa taka   limekuwa  likifanya  shughuli za  kilimo na  kusomba  matofali  na kuacha shughuli za  kukusanya taka hali inafanya taka kurundikana na kuufanya mji wa Maswa  kuwa  mchafu.

Sauti za baadhi ya wajumbe wa Baraza la Mamlaka ya Mji Maswa wakichangia hoja
Wajumbe wa Baraza la Mamlaka ya Mji Maswa wasikiliza hoja wakati wa kikao

Caroline  Shayo  ni  Mwenyekiti wa  mamlaka ya mji mdogo Maswa  akamtaka  Mkurugenzi  Mtendaji wa  Halmashauri  ya Wilaya  ya  Maswa  kutoa  ufafanuzi wa kina  kwanini trekta  imebadilishiwa  matumizi  yake yaliyokusudiwa ya kukusanya  na  kuzoa taka na  badala yake linafanya kazi za  kilimo na shughuli za  ujenzi  na  kuacha  uchafu ukikithiri  katika  Mamlaka ya mji huo.

Sauti ya Caroline Shayo -Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Maswa

Akitolea  ufafanuzi  kuhusu trekta  la kuzoa  taka  kubadilishiwa matumizi, Kaimu  Mkurugenzi  Mtendaji wa  Halmashauri ,   Vivian  Christian  amesema  kuwa  trekta  wamesharikabidhi  kwa Mtendaji wa  mamlaka,  hivyo  wanapolihitaji  wawasiliane  ili  kujua lipo sehemu gani  na  linafanya  kazi  ipi  na  kwa muda  gani

Sauti ya Vivian Christian kaimu DED Maswa akitoa ufafanuzi wa trekta
Aliyeshika mic ni Veronica Mbiha -Mtendaji wa mamlaka ya mji mdogo Maswa akifafanua hoja

Aidha  akitoa  taarifa  utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa niaba ya  Mkurugenzi  mtendaji  wa mamlaka ya mji mdogo Maswa   Bi  Veronica   Mbiha,   ndugu Keneth  Julius   amesema  kuwa  ukusanyaji  wa  mapato umeongezeka  ambapo  katika  kipindi cha robo ya kwanza mamlaka imekusanya  zaidi ya  shilingi Milioni  76.6  sawa  na  asilimia  76.6 % ya makisio ya  makusanyo yote.

Sauti ya Keneth Julius akitoa taarifa ya utekelezaji kwa niaba ya mtendaji wa mamlaka ya mji

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi – ccm  Wilaya ya  Maswa  ndugu  Onesmo  Makota amewapongeza  mamlaka  kwa  jitihada za ukusanyaji wa  mapato hivyo  kuwataka  waongeze  bidii  zaidi  ili  kufikia  malengo  na  hatimae kupanda  kuwa  Halmashauri ya  Mji.

Sauti ya Onesmo Makota -Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswa
Aliyesimama (ameshika mic ) ni Onesmo Makota mwenyekiti wa CCM – Maswa
Aliyesimama (ameshika mic ) ni Vivian christian kaimu DED Maswa akifafanua jambo wakati wa kikao