Sibuka FM

Wananchi Wilayni Maswa wajitokeza kuchangia  Damu, watoa wito kwa Jamii

24 November 2025, 11:41 am

mwananchi akiwa katika zoezi la kuchangia damu

Mahitaji ya damu katika Hospitali ya wilaya yetu ni makubwa ukilinganisha na upatikanaji wake, hivyo natoa wito kwa jamii kujitokeza kuchangia damu ili kuokoa maisha ya watanzania wenzetu. ” Peter Shimba Mratibu wa damu salama hospitali ya wilaya ya Maswa “

Wananchi  Wilayani  Maswa, mkoani Simiyu wamejitokeza  kwa  wingi katika  zoezi la  uchangiaji wa  Damu ili kuokoa  maisha  ya  watu  wengine  wenye  uhitaji  wa  Damu,  ambapo zoezi hilo  likiratibiwa  na  Kituo cha  Afya  cha  Barikiwa  kilichopo maswa  mjini maeneo ya  mnadani.

Wakizungumza  na  Sibuka fm  baada  ya  kuchangia  damu, wananchi  hao wamesema  kuwa zoezi ni zuri hivyo wananchi wengine  wajitokeze  kuchangia  damu  pamoja  upimaji  wa  magonjwa  mbalimbali yakiwepo magonjwa  yasiyo yakuambukizwa

sauti za baadhi ya wananchi walioshiriki kuchangia damu
wananchi wakiwa katika foleni ya kupama huduma ya vipimo vya afya

Dr  Ashley  Lucas  ni  Mkurugenzi  wa  kituo  cha  afya  cha  Barikiwa  amesema  kuwa  wameamua  kuja  na  kampeni  hiyo  lengo ni  kusogeza  huduma  za  afya  kwa  jamii na kutambua  hali zao za  kiafya kwa kupima bila  gharama  yoyote  hivyo wananchi wajitokeze 

sauti Dr Ashley Lucas Mkurugenzi wa kituo cha afya cha Barikiwa

Kwa  upande  wake  mratibu wa  Damu  salama  kutoka  Hospitali ya  wilaya ya Maswa  Dr  Peter Emmanuel  Shimba  amesema  mahitaji ya  damu  ni  makubwa  ukilinganisha  na  upatikanaji wake  hasa  wakati ambao  shule zikiwa  zimefungwa  hivyo jamii  iguswe  kuchangia huduma hiyo ya damu

sauti ya Peter Shimba – Mratibu wa damu salama hospitali ya Maswa

Aidha  Dr  Shimba  ametoa  wito  kwa  jamii  kujitokeza  kuchangia  damu  kwa  mahitaji ni  makubwa  hasa  watoto  wenye seli mundu, akina  mama wajawazito wakati wa  kujifungua pamoja  na  watu  wanaopata  ajali  huku  akiwashuru  wadau  wa  Kituo  cha  Afya  cha  Barikiwa  kwa  kutoa  sapoti pamoja  na  kuratibu  zoezi  hili  muhimu  linalolenga  kuokoa  maisha  ya  Watanzania

sauti ya Peter Shimba – Mratibu wa damu salama hospitali ya Maswa
pichani watatu kulia ni Dkt Vicent Anney DC Maswa akishuhudia fainali ya mashindano ligi daraja la 4 yaliyodhaminiwa na Kituo cha afya cha Barikiwa

Katika  kampeni  hiyo  iliyoambatana  na  mashindano ya fainali ya  mpira wa  miguu  yaliyodhaminiwa  na  kituo hicho  cha  Barikiwa, Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Dkt  Vicent  Naano  Anney akatoa  wito  kwa  Jamii  kuwa  na  tabia  ya  kupima  afya  huku akaahidi kuanzisha  ligi  nyingine  ndogo ambayo  kilele  chake  kitakuwa  tarehe  9  Disemba   siku ya  Uhuru  wa  Tanganyika

sauti ya Dc maswa Dkt Vicent Anney akizungumza baada ya mashindano ya mpira kumalizika
picha mwenye mpira ni Dkt Vicent Anney Dc Maswa akiwa na Mkurugenzi wa Kituo cha afya cha Barikiwa Dr Ashley Lucas (mwenye suluali ya pinki )