Sibuka FM

Mradi wa mabadiliko ya tabia nchi  kuwaneemesha wakulima na wafugaji Simiyu

23 November 2025, 3:07 pm

washiriki wa mafunzo (wakulima na wafugaji ) kutoka halmashauri sita za mkoa wa simiyu wakiendelea kupata mafunzo kupitia Mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi– Simiyu Climate Resilience Project SCRP Picha na Nicholaus Machunda

Tunatoa mafunzo kwa wakulima na wafugaji tuliowachagua kutoka wilaya tofauti za mkoa wa simiyu tunawafundisha namna ya kutunza uoto wa asili na kupanda miti (ngitili ) kwa ajili ya malisho ya mifugo yao.. “Raymond Makanga- SCRP “

Serikali  Mkoa  wa  Simiyu inatarajia  kutoa Hati za kimila  6000 kwa  wakulima  na  wafugaji  kutoka Halmashauri  sita  za  mkoa   ili kuongeza thamani ya maeneo  yao  na  kuchochea  utunzaji wa  mazingira  kupitia  mradi wa mabadiliko ya  tabia  nchi.

Akizungumza  na  waandishi  na  waandishi wa  habari  wakati wa  mafunzo ya  kuwajengea  uwezo  wakulima  na  wafugaji, Meneja  mradi  wa  kukabiliana  na  mabadiliko ya  tabia  nchi  mkoa  wa  Simiyu Mhandisi  Gogadi Mgwatu  amesema  kuwa   mradi  huo  unakusudia  kurejesha  uoto  wa  asili  kwa  kupanda miti  na  nyasi za  malisho.

sauti ya Gogadi Mgwatu- meneja mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi- Simiyu
wakulima na wafugaji wakifuatilia mafunzo kuhusu mabadiliko ya tabia nchi

Mhandisi  Kahabi  Medard ni afisa  kutoka  mradi  wa  kukabiliana  na  mabadiliko ya tabia  nchi  anaeleza  maeneo  matatu  ambayo mradi  umejikita  huku  akitaja  manufaa  yatakayopatikana  kutokana  na  mradi   huo  ambao  upo  chini  ya Wizara  ya maji.

sauti ya Kahabi Medard afisa kutoka mradi wa SCRP

Kwa  upande  wake  Raymond  Makanga  kutoka  Simiyu  Climate Resilience  Project- SCRP   amesema  kuwa  wametoa  mafunzo kwa  wakulima na  wafugaji  zaidi ya  200 kutoka  Halmashauri  Sita  za  mkoa  wa  Simiyu ili kwenda  kuhamasisha  utunzaji  wa  mazingira  na kurejesha  uoto wa  asili

sauti ya Raymond Makanga afisa kutoka mradi wa SCRP

Nao  baadhi ya  wakulima  na  wafugaji  walioshiriki  mafunzo  hayo  wameishukuru  serikali  ya  awamu ya  sita  chini  ya  Mhe   Rais  Dkt  Samia  suluhu  Hasan kwa mradi  huo utaoenda  kuondoa  migogoro ya  ardhi kati ya  wakulima  na  wafugaji  kwani maeneo yatapimwa  na  kupatiwa  Hati  pamoja  kupanda  miti ya  marisho  kwa  wafugaji

sauti za baadhi ya wakulima na wafugaji kutoka halmashauri za mkoa wa simiyu
Gogadi Mgwatu -Meneja mradi SCRP
washiriki wa mafunzo
Miti kwa ajili ya kuhifadhi uoto wa asili