Sibuka FM

Msimu wa kilimo cha Pamba wazinduliwa  Maswa, Dc Anney  atoa maagizo

21 November 2025, 8:51 pm

Aliyesimama ni Mkuu wa Wilaya ya maswa Dkt Vicent Naano Anney akizungumza wakati wa hafla ya Uzinduzi wa msimu wa kilimo cha Pamba 2025/2026. Picha na Nicholaus Machunda

Wataalamu wa kilimo sitaki kuwaona maofisini nataka niwakute mashambani mkiwasaidia wakulima kuzalisha kwa tija ili kuondokana na malalamiko ya kushuka kwa bei ya pamba angalau mkulima azalishe kilo elfu moja kwa ekari Moja ” DC Vicent Naano Anney ”

Msimu wa Kilimo cha  zao la Pamba 2025/2026  umezinduliwa  rasmi  wilayani  Maswa  Mkoa  wa  Simiyu  kwa  ajili ya  wakulima kuanza  zoezi  la  upandaji  wa  mbegu za  Pamba  kwa mjibu wa  kalenda ya  Bodi ya  pamba Tanzania pamoja kilimo cha  mazao mengine.

 Akizungumza wakati wa  uzinduzi huo, Mkuu wa  Wilaya ya  Maswa  Mhe,  Dkt  Vicent  Naano  Anney   na  kutoa  maagizo kwa maafisa  kilimo ngazi ya  Wilaya  na  kata kuhakikisha  wanatoka  maofisini  na  kwenda  kuwahudumia  wakulima  ili  kuongeza  tija ya  uzalishaji

sauti ya DC Maswa Mhe Vicent Anney akizungumzia uzalishaji wa tija

Aidha   Mhe  Anney  amesema  kuwa  mara  nyingi  wakulima  wamekuwa  wakipata  hasara  katika  zao  za  Pamba  kwakuzalisha kilo chache  za  pamba hivyo  kuwataka  walime  kitaalamu  na  kufuata  kanuni bora  za  kilimo  cha  zao  hilo  huku  akitoa  mifano ya maeneo  mengine yaliyoweza  kuzalisha  zaidi ya  kilo elfu moja  kwa ekari moja

sauti ya DC Maswa Mhe Vicent Anney akizungumzia uzinduzi wa pamba
Dc Anney (aliyeshika Jembe) akipata maelezo kutoka mtaalamu wa kilimo(aliyeshika mic) wakati wa uzinduzi wa msimu wa kilimo

Akitoa  taarifa  kwa  mgeni  rasmi  katika  uzinduzi  huo, Kaimu  mkuu  wa  division ya Kilimo  Halmashauri ya wilaya Maswa  ndugu  Gimu Yohana Mbabula  ametaja malengo  ya kilimo kwa msimu wa  mwaka huu pamoja na  mikakati ya Halmashauri  katika  kuongeza  tija ya uzalishaji  wa zao la pamba

sauti ya Gimu Yohana Mabula mtaalamu wa kilimo halmashauri ya Maswa
Wakulima wakipata elimu kuhusu kifaa ya kupima udongo wakati wa uzinduzi wa msimu

Baadhi ya  wakulima  waliohudhuria  uzinduzi  huo wamezungumza  na  SIBUKA  FM na  kuelezea matarajio  yako katika  msimu  huu  baada  ya  kupewa elimu na maelekezo  kuhusu   namna  ya  uzalishaji  wenye  tija  katika  zao la  Pamba

sauti za baadhi ya wakulima waliohudhuria wakizungumzia walivyopata elimu ya pamba

Naye  diwani  mteule  wa  kata ya  Mwamashimba  kupitia  chama cha  mapinduzi – ccm  ambapo zoezi la uzinduzi  wa  msimu  wa  kilimo  cha  Pamba  kwa  mwaka  2025/2026  ndugu  Saida  Daudi Dila ameishukuru  Serikali  kwa  kutoa zana za kilimo na pembejeo  za  ruzuku  kwa  wakulima  ili  kuleta  hamasa  ya  kulima  zao la  pamba

sauti ya Saida Daudi diwani mteule akiishukuru serikali kwa kuinua zao la pamba