Sibuka FM

 Dkt  Lugomela ahitimisha kampeni za uchaguzi  kwa kishindo- Maswa

28 October 2025, 11:35 am

Wananchi waliojitokeza kusikiliza kampeni za mgombea Ubunge Jimbo la maswa mashariki Dkt George Lugomela Picha na Nicholaus Machunda

Nimezunguka kata zote 19 za Jimbo la Maswa mashariki nimesikiliza kero na kujionea changamoto mbalimbali hivyo mkinipa ridhaa ya kuwa mbunge wenu nitaenda kuzitatua ” Dkt George Lugomela”

Mgombea Ubunge Jimbo la Maswa  Mashariki Mkoani Simiyu  kupitia  chama cha  mapinduzi –ccm  Dkt   George Venance Lugomela amehitimisha  kampeni zake za  uchaguzi kwa kishindo  baada  ya  kuzunguka  kata  zote  kumi na tisa  na kusikiliza  kero na  changamoto za  wananchi wa  jimbo hilo.

Katika  ahadi  zake  Dkt  Lugomela  amesema  kuwa  endapo  wananchi wa  Maswa  watampa  ridhaa  ya  kwenda  kuwawakilisha  huko  Bungeni  atahakikisha  suala  la  maji  anaanza  nalo kwani  ndio changamoto  kubwa  kwa  wananchi wa  Maswa  pamoja  na  sekta  nyingine  nyingine za  Afya,  Elimu, Kilimo, Mifugo na  Miundombinu

sauti ya Dkt George Lugomela wakati wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi

Kwa  upande  wake  mwenyekiti wa  chama cha  Mapinduzi Mkoa  wa  Simiyu  Ndugu  Shemsa  Mohamed  amewaomba  wana  Maswa  wakichague  chama  cha  Mapinduzi  kuanzia  nafasi ya  Rais,  Wabunge na  Madiwani kwani  ndio  chama  pekee  kinachowaletea  maendeleo  wananchi  hivyo  ni  vyema  uweka  mafiga  matatu.

sauti ya Shemsa Mohamed- Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Simiyu
Baadhi ya wagombea udiwani kata za mjini maswa wakiomba kura kwa wananchi

Stanslaus  Nyongo  ni  mjumbe  wa  Halmashauri  kuu ya  chama cha Mapinduzi – NEC   na  mbunge  mstaafu wa Jimbo la Maswa  mashariki  amesema  kuwa  Mhe  Dkt  Rais Samia  Hasani amefanya  mambo makubwa  ya  maendeleo  katika  wilaya  ya  Maswa   hivyo wana maswa  wakampe  kura  nyingi za  kutosha  ili aendelee  kuleta  fedha  za  maendeleo

sauti ya Stanslaus Nyongo -Mjumbe wa NEC akimnadi Dkt Lugomela