Sibuka FM
Sibuka FM
26 October 2025, 3:30 pm

Siku ya uchaguzi tarehe 29 mwezi Oktoba 2025, nawasihi wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa vituo mkatoe vipaumbele kwa makundi maalumu ya watu wenye ulemavu, wazee, wajawazito na akina mama wanaonyonyesha “Julius Ikongora John Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Maswa”
Na Mwandishi wetu
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Maswa Mashariki na Maswa Magharibi Mkoani Simiyu amewataka wasimamizi wa Uchaguzi kwenye vituo vya kupigia kura kuhakikisha wanatoa kipaumbele kwa makundi maalumu ya Wazee, Wajawazito, watu wenye Ulemavu na akina mama wanaonyonyesha
Hayo ameyasema leo Oktoba 26, 2025 wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa Wasimamizi na Wasimamizi wasaidizi wa vituo vya kupigia kura na kuwataka wazingatia makundi hayo ili kuepuka usumbufu kwenye vituo vya kupigia kura
Ikongora ameongeza kuwa wasimamizi hayo wa vituo vya upigia kura wanapaswa kutunza siri za tumekulingana na kanuni za Tume huru ya Taifa ya uchaguzi hivyo kukiuka viapo kunaweza kuwatia hatia kwa mjibu wa sheria, miongozo na katiba ya Tume

Nao wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa Vituo vya kupigia kura wanaeleza namna walivyopokea mafunzo na kuahidi kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, Kanuni na Miongozo ya Tume huku wakitoa kipaumbele kwa makundi maalumu, wananchi wajjitokeze kwa wingi siku ya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ifikapo Oktoba 29, 2025
Uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utafanyika tarehe 29, Oktoba, 2025 ambapo katika Jimbo la Maswa mashariki na Jimbo la Maswa magharibi, Jumla ya wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa Vituo vya upigia kura 2043 wamepewa mafunzo kwa ajili ya usimamizi wa zoezi hilo.


