Sibuka FM

Leseni ya udereva, Paspoti na NIDA kumchagua kiongozi

22 October 2025, 2:46 pm

Kwenye picha ni muonekano wa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Maswa Mashariki na Maswa Magharibi wilayani Maswa,Julius John akizungumza jambo na waandishi wa habari kuelekea siku ya uchaguzi Picha kwa hisani

Kuchagua kiongozi unayemtaka ni takwa la kikatiba katika kuleta maendeleo kwenye eneo husika ndiyo maana sasa unapofika uchaguzi tunawataka wananchi waweze kuitumia hiyo haki ya kuchagua kiongozi wamtakao wenyewe”.

Na,Daniel Manyanga 

Wilayani Maswa mkoani Simiyu imeelezwa kuwa wale wote waliopoteza kadi ya kupigia kura watatumia Leseni ya udereva,Kitambulisho cha Taifa(NIDA) na hati ya kusafiria(Paspoti) wakati wa kupiga kura siku ya uchaguzi ili nao waweze kutimiza takwa la kikatiba la kumchagua kiongozi kwa ngazi ya Udiwani,Ubunge na Urais mnamo tarehe 29.10.2025. 

Akizungumza na Sibuka Fm msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Maswa Mashariki na Maswa Magharibi wilayani hapo,Julius John ametaja vitu vya kuzingatia kwa wale ambao wamepoteza kadi ya kupigia kura siku hiyo ya uchaguzi. 

Sauti ya msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Maswa Mashariki na Maswa Magharibi akielezea namna ambavyo watapiga kura waliopoteza kadi ya kupigia kura

Julius ameongeza kuwa vituo vitakavyotumika kupigia kura ni vile vilivyotumika wakati wa zoezi la kujiandisha katika daftari la kudumu la wapiga.

Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Maswa Mashariki na Magharibi akizungumzia vitua vitakavyotumika wakati wa kupiga kura

Katika hatua nyingine msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Maswa Mashariki na Maswa Magharibi,Julius John amewaomba Wananchi kuhakiki majina yao katika vituo walivyojiandikishia kabla ya siku ya uchaguzi. 

Sauti ya Julius John akitoa wito kwa wananchi kuhakiki majina yao kabla ya uchaguzi