Sibuka FM

ADA TADEA: Mkituchagua, Wazee  watalipwa  posho kila mwisho wa mwezi

22 October 2025, 12:29 pm

Picha ni wananchi wa kata ya Malampaka wilayani Maswa wakiwa na mabango ya mgombe Urais kupitia chama cha ADA TADEA- Mhe George Busungu picha na Nicholaus Machunda

Wazee ni hazina ya Taifa maana wamelitumikia kwa nguvu zao zote hivyo tunapaswa kuwajali na kuwatunza ili wasiwe omba omba na kunyanyasika– ” Georges Busungu -Mgombea Urais Ada tadea

Mgombea  Urais  kupitia  Chama cha African Democratic  Alliance Party ( ADA  – TADEA) Mhe  Geoerges  Busungu  amesema  kuwa  endapo wananchi   watakipa  ridha  chama  hicho  kuongoza   Nchi  kitahakikisha  wazee wote  wanalipwa  Posho  ya  kujikimu ili kuepusha  tatizo  la kuwa  Omba omba

Mhe  Busungu  amesema  hayo  wakati  wa  Mkutano wa  kampeni  za  kunadi  Ilani  ya  chama  hicho ulifanyika  katika  kata  ya  Malampaka  wilaya  ya Maswa, Mkoa  wa  Simiyu  na  kusisitiza  kuwa   wazee  ndio  hazina  ya  Taifa  hivyo  ni  muhimu kuwajali

sauti ya Georges Busungu-Mgombea Urais kupitia chama cha ada tadea

Mgombea  Urais  huyo  ameongeza  kuwa  Tanzania  inaweza  kubadilika  iwapo  wananchi  tutaamua  kubadilisha fikra  zetu ili  kuleta  mapinduzi  ya  Kiuchumi  ambapo  makundi  ya  Wakulima, wafugaji, Wafanyakazi  na  wafanyabiashara  yatahusishwa  kikamilifu

sauti ya Georges Busungu-Mgombea Urais kupitia chama cha ada tadea
Katibu mkuu wa chama cha Ada tadea ndugu Salehe Mohamed Msumari (aliyeshika Mic ) akimnadi mgombea udiwani kata ya malampaka Charles Mwinuka

Kwa  Upande  wake Katibu  Mkuu  wa  Chama  hicho  Ndugu  Salehe  Mohamedi  Msumari amesema  kuwa  endapo wananchi  watakiweka  madarakani  kipaumbele  kitakuwa  Afya  bure, Elimu  bure  hadi  chuo kikuu  na  siyo  kama  ilivyokwasasa  afya  bure  lakini  watu  wanaendelea  kuchajiwa fedha  za  matibabu

sauti ya Salehe Msumari-Katika mkuu wa chama cha Ada tadea

Charles  Mwinuka  ni  Mgombea  Udiwani  kata  ya  Malampaka  kupitia  Chama  cha  Ada Tadea  amewahakikishia  maendeleo   katika  Mji  huo  endapo  watamchagua  kuwa  mwakilishi wao  kwa  ngazi  ya  kata  hivyo  wawe  na  imani  nae.

sauti ya Charles Mwinuka Mgombea udiwani Ada tadea kata ya Malampaka
Picha za matukio mbalimbali ya kampeni za chama cha Ada tadea katika kata ya malampaka wilaya ya Maswa