Sibuka FM

DC Anney awaalika wananchi Maswa kupata huduma za kibingwa

8 October 2025, 8:48 am

Picha Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt Vicent Anney akiwa na timu ya madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili -Mlonganzila baada ya kuripoti ofisini kwake tayari kwa kutoa Huduma za kibingwa katika Hospitali ya Barikiwa-Maswa. Picha na Nicholaus Machunda

Niwapongeze sana Hospitali ya Barikiwa kwa kutekeleza azima ya Serikali ya kusogeza huduma kwa wananchi hivyo niwasihi wananchi wa Maswa na viunga vyake waitumie vyema fulsa hii ya Ujio wa Kambi ya Madaktari Bingwa ” Dkt Vicent Naano Anney Mkuu wa Wilaya ya Maswa “

Mkuu wa  Wilaya  ya  Maswa   Mhe  Dkt  Vicent  Naano  Anney  amewataka  Wananchi  kutumia  fulsa  ya  ujio wa  madaktari bingwa  katika Hospitali ya  Barikiwa iliyopo wilayani  hapo  ili kupata matibabu ya  magonjwa  mbalimbali.

Mhe  Dkt  Anney  ametoa  wito  huo baada ya Madaktari  bingwa  hao  kuripoti ofisini  kwake  wakitokea  Hospitali ya Taifa Muhimbili  – Mloganzila   kwa  ajili ya kuja  kutoa  huduma za kibingwa  kwa  wananchi  wa Wilaya  ya  Maswa na  Wilaya  jirani za  mkoa  wa  simiyu

sauti ya Mkuu wa Wilaya Dkt Vicent Anney akitoa wito kwa wanachi kujitokeza

Aidha   Mkuu wa  Wilaya  ameipongeza  Hospitali ya  Barikiwa  kwa  Ubunifu  waliofanya  wa  kuleta  huduma za Madaktari  bingwa  ili kusogeza  huduma kwa Wananchi na  kupunguza gharama  za  matibabu ambazo wangezipata katika Hospitali kubwa za rufaa na Kanda

sauti ya Mkuu wa wilaya Dkt Vicent Anney akiwapongeza Hospitalia ya Barikiwa
Mkurugenzi wa Hospitali ya Barikiwa Dr Ashley Lucas

Dr  Hildegard  Ashley Lucas  ni Mkurugenzi  wa Hospitali ya  Barikiwa  amesema kuwa  lengo  la kuleta  madaktari  bingwa hao  ni kusogeza  huduma  kwa  wananchi  na  kusaidia  upatikanaji wa  huduma  za  kibingwa  kwa  gharama nafuu  na zenye  ubora  zaidi  huku  Bima  mbalimbali za  afya  zikipokelewa

Hii hapa sauti ya Dr Hildegard Ashley Lucas akizungumzia lengo la ujio wa madaktari bingwa

Nao  baadhi ya  madaktari Bingwa  kutoka  Hospitali ya Taifa Muhimbili -Mloganzila wamesema  kuwa  wapo  Maswa  katika  Hospitali ya  Barikiwa  kwa  Kambi  Maalumu   ya  Magonjwa ya  mfumo wa  ndani, wagonjwa ya  akina  mama, mfumo  wa  Uzazi , kinywa  na  Meno,  Upasuaji   na  mifupa   hivyo wananchi wajitokeze  kupata  vipimo na  matibabu bora

sauti ya Dr Erick Maro Mumba- Daktari bingwa wa Upasuaji kutoka Hospt ya Taifa Mloganzila
Mkuu wa Wilaya ya Maswa akizungumza na timu ya Madaktari bingwa ofisi kwake
madaktari bingwa wakiendelea kutoa huduma ya kipimo cha mfumo wa hewa na chakula