Sibuka FM

Mkulima aliyepata kilo zaidi 3000 za Pamba kwa ekari 1afunguka siri ya mafanikio

1 October 2025, 7:03 pm

Mzee Kuseka Matonange ni mkulima kutoka kijiji cha Nyansalala kata ya Bukondo wilaya ya Geita akielezea siri ya mafanikio ya kupata kilo zaidi ya elfu tatu kwa ekari moja

Nimekuwa mkulima wa Pamba kwa muda mrefu sasa lakini zamani nilikuwa nalima kiholela sana hivyo sikupata mavuno mazuri Lakini baada ya kupata elimu sahihi na Ushauri kutoka kwa wataalamu wa kilimo, mwaka huu nimepata kilo zaidi ya elfu tatu za Pamba kwa ekari moja Ninaishukuru sana Serikali kupitia Bodi ya Pamba Tanzania-TCB

Inaelezwa  kuwa  mkulima kupata  zaidi ya  kilo elfu tatu kwa  ekari moja ni  kama  ndoto  lakini imewezekana kwa mkulima Kusekwa Matonange  kutoka  Kijiji cha Nyansalala  kata  ya  bukondo  Wilaya ya  Geita  Mkoa  wa  Geita   ambaye  katika  msimu  huu kilimo  wa  2024/2025 amepata  Kilo  zaidi  ya  elfu tatu  ikilinganishwa  na  mwaka  jana  ambapo mkulima  huyo  alipata  zaidi ya kilo zaidi ya  elfu  mbili.

Mzee  Matonange  anaeleza  siri  za  mafanikio katika  mavuno  hayo  licha  ya  kupata  changamoto  za  hapa  na  pale,  lakini  anasisitiza  kufuata  kanuni za  kilimo  cha  pamba  pamoja  na  ushauri  anaopewa  na  wataalamu  wa  kilimo  huku akitoa  shukurani  nyingi  kwa  Bodi ya  Pamba Tanzania – TCB  kwa jitihada  zinazofanyika  kwa  lengo la  kumuinua mkulima  na  kuongeza  Uzalishaji

hii hapa sauti ya mzee Kusekwa Matonange akielezea siri ya mafanikio katika zao la Pamba

Elisha  Athanasi  ni  kijana  anayejishirikisha  na  zao la pamba huku akijifunza  kutoka  kwa  mzee kusekwa Matonange   anatoa  wito  kwa  vijana kujikita  katika  zao  hilo kwasababu kinainua  wakulima  kama  watafuata  kanuni  na  ushauri  wa  wataalamu  wa  kilimo

sauti ya Elisha Athanas -mkulima kutoka kijiji cha nyansalala wilaya Geita
mkulima akiwa amesafisha shamba lake kwa ajili ya mandalizi ya msimu wa kilimo cha Pamba
mkulima baada ya kuvuna pamba yake aliyolima kwa kufuata kanuni za kilimo cha pamba