Sibuka FM

DC Igunga atoa maagizo kuelekea msimu wa kilimo cha  pamba

1 October 2025, 8:11 am

Mkuu wa wilaya ya Igunga Bi Sauda Mtondoo akizungumza na waandishi wa Habari za Pamba alivyojipanga katika uzalishaji wa zao la pamba kwa msimu wa 2025/2026

Kama mnavyojua wilaya ya Igunga inalima zao la Pamba na kuzalisha kitalu mbegu hivyo Serikali inafanya jitihada zote kuhakikisha uzalishaji unaongezeka mwaka hadi mwaka hivyo zao hili tunalipa kipaumbele kwasababu ni zao la kibiashara.” Sauda Mtondoo DC Igunga “

Na Nicholaus Machunda

Mkuu  wa  Wilaya  ya  Igunga  Mkoani  Tabora  Mhe  Bi  Sauda  Mtondoo   ametoa  maagizo  kwa  wakulima wa zao la Pamba  kuhakikisha  wanafuata  kanuni  bora  za  kilimo  cha zao  hilo ili  uleta  tija na kujikwamua  kiuchumi.

Mhe  Mtondoo  ametoa   maagizo  hayo  wakati  akizungumza  na  Waandishi  wa  Habari  za  Pamba  na  Mazingira  baada  ya  kumtembelea  ofisini  kwake   ili kutaka  kujua  Wilaya  yake  imejipangaje  katika  uzalishaji  Wenye tija  katika  zao la  Pamba  maarufu  kwa jina la dhahabu  nyeupe

hii hapa sauti ya Sauda Mtondoo Mkuu wa Wilaya ya Igunga- Tabora

Mhe  Mtondoo ameongeza   kuwa   Wilaya  ya  Igunga  tayari  imeshapata  mgao  wa  mbegu  kwa  ajili  ya  kilimo  cha  Msimu  wa  2025/2026 hivyo  kuwaondoa  wasi wasi  wakulima  kuhusu  upatikanaji  wa  mbegu  huku  akiishukuru  Serikali  na  Bodi  ya  Pamba  Tanzania  kwa  kuleta  mbegu  kwa  wakati

hii hapa sauti ya Sauda Mtondoo Mkuu wa Wilaya ya Igunga- Tabora

Kwa  upande  wake afisa  kilimo  kutoka  mradi  wa  Jenga  kesho iliyo bora ( Buld  Better Tommorow – BBT ) Nice  Thomas  amezungumzia  ujio wa mbolea   Ukaa  inayotengenezwa  kutokana  na  masalia  ya  miti  ya  Pamba inavyoweza  kuongeza  tija  katika  Uzalishaji  wa  Pamba

sauti ya Nice Thomas afisa kilimo wa mradi wa BBT
Teknolojia mpya ya mbolea ukaa inayotengenezwa kutokana na masalia ya pamba

Baadhi  ya  wakulima  waliozungumza  na  Sibuka  Fm  wamesema  kuwa  elimu ya mbolea ya  Ukaa itaenda  kuwaongezea  Uzalishaji  wa Tija  huku  wakiwaomba  wakulima  wenzao  ambao bado  hawajatoa  masalia  ya  pamba  watoe   mapema  ili  kufanya  maadalizi  ya shamba  kwa  ajili  ya  kilimo cha  pamba

sauti za wakulima wa zao la pamba wilayani Igunga- Tabora
wakulima wakionesha namna ya kuandaa mbolea ukaa inayotokana na masalia ya pamba