Sibuka FM

Mashimba Ndaki azindua kampeni za ubunge- Maswa magharibi

22 September 2025, 10:13 pm

Mgombea Ubunge Jimbo la Maswa magharibi kupitia chama cha mapinduzi -ccm Mashinda Ndaki wakati wa uzinduzi wa Kmapeni. Picha na Nicholaus Machunda

Niingia madarakani nitafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha mradi wa maji ya ziwa Viktori unakamilika maana utazifaidisha kata zangu za Zanzui, mwamashimba, Buchambi na kata ya Busangi ambazo zinachangamoto ya Maji ” Mashimba Ndaki -mgombea ubunge maswa magharibi -ccm “

Mgombea  Ubunge  Jimbo  la  Maswa  Magharibi lililopo wilayani  Maswa Mkoani Simiyu  kupitia  chama cha Mapinduzi  CCM,  Mhe  Mashimba  Mashauri  Ndaki  amezindua  rasmi  kampeni  ili  kuomba  ridha  ya  wananchi  huku akitaja  vipaumbele  atavyoanza  navyo  baada  ya  kuchaguliwa  katika uchaguzi  utakaofanyika mwisho wa  mwezi  Oktaba , 2025

Mhe  Mashimba  anaomba  kukutea  nafasi yake kwa  kipindi  kingine  ili aendelee  kuwapambania  hasa  mradi  wa  maji  kutoka  ziwa  viktoria  ambayo  ndio  itakuwa  mwarobaini ya  changamoto ya  maji katika  Jimbo lake.

sauti ya Mashimba Ndaki akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni

 Aidha  Mhe  Mashimba  amesema  kuwa  wakati  anapata  ubunge  jimbo lilikuwa  chini  kimaendeleo hasa  katika  huduma  za  upatikanaji  wa  Maji baada  ya  kuingia  alisimamia  maeneo  mengi  yakapata  maji  na  kupunguza  adha  waliyokuwa  wanapata  wananchi  wake.

sauti ya Mashimba Ndaki akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni
Mwenyekit wa ccm wilaya ya Maswa Ndugu Onesmo Makota akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni

Kwa upande  wake  mgeni  rasmi  katika  uzinduzi wa  kampeni  hizo  ambae  pia  ni Mwenyekiti  wa  ccm  wilaya  ya  Maswa  Mwl  Onesmo  Makota  amesema  kuwa  chama  kitafanya  kampeni  za  kistaarabu bila  vurugu  wala  ugomvi  hivyo wananchi wakiamini  ili  kudumisha  amani  tuliyo  nayo

sauti ya Onesmo Makota mwenyekiti wa ccm wilaya ya Maswa

Dkt  George  Lugomela   ni  Mgombea  ubunge  Jimbo la Maswa  mashariki  akapata  nafasi ya  kumuombea  kura  Mgombea ubunge Jimbo la  Maswa Magharibi   Mhe, Mashimba  ndaki  huku  akisema  wajumbe wa  Maswa  Magharibi  hawakukosea  kumchagua  kwani  ni  mchapaka  kazi  na  mfuatiliaji  wa  maendeleo  kwa  wananchi  wake

sauti ya George Lugomela akimnadi mashimba ndaki wakati wa uzinduzi wa kampeni
wananchi wakiwa wanasikiliza sera za mgombea ubunge jimbo la maswa magharibi wakati wa uzinduzi wa kampeni katika kijiji cha Masela, kata ya Masela
Wakwanza kulia ni Mashimba ndaki mgombea ubunge maswa magharibi kushoto kwake ni mgombea ubunge maswa mashariki George Lugomela wakati wa uzinduzi