Sibuka FM

Wananchi wafurika kupata huduma za Madaktari  Bingwa Hospitali ya Maswa

22 September 2025, 7:14 pm

Picha ni wananchi wakiwa katika foleni ya kusubiri kupata huduma kutoka kwa madaktari bingwa katika Hospitali ya wilaya ya Maswa. Picha na Nicholaus Machunda

Ujio wa kambi ya madaktari bingwa katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa utasaidia kusogeza huduma kwa wananchi ambazo walitakiwa wazipate katika Hospitali kubwa za rufaa na kanda lakini kwa sasa zinatolewa na Hospitali yetu ya Wilaya ” Dc Maswa Dkt Vicent Anney “

Wananchi  wa  Wilaya  ya  Maswa  Mkoa wa  Simiyu  wamejitokeza  kwa  wingi  kupata  huduma  za  Madaktari  bingwa  zilizoletwa  na  Halmashauri ya  wilaya kwa lengo  kusogeza  huduma  za  kibingwaa  kwa  wananchi

Wananchi  hao  wameishukuru  serikali  kwa  uwepo  wa  huduma  hizo  za  kibingwa  kwenye Hospitali ya  wilaya kwani  hapo awali walikuwa wanatumia  gharama  kubwa  kwenda  hospitali   na mikoa na  za  rufaa  kwa  ajili  ya  kupata  huduma  hizo

sauti za wananchi wakiishukuru Serikali kwa kuleta madaktari bingwa katika Hospitali ya Maswa
Mganga Mfawidhi Hospitali ya wilaya ya Maswa Dr Deogratius Mtaki akizungumzia Ujio wa Madaktari Bingwa

Dr  Deogratius  Mtaki  ni  Mganga  mfawidhi  katika  Hospitali ya  wilaya ya  maswa amesema  kuwa  huduma  zinazotolewa  na  Madaktari  bingwa  hao ni  pamoja  matibabu ya Macho,  Masikio, Pua, Koo, Upasuaji  mkubwa , upasuaji  mdogo na  huduma za  Uzazi  kwa wanawake

sauti ya Dr Mtaki akizungumzia ujio wa madaktari Bingwa

Aidha  Dr  Mtaki  ameishukuru  serikali ya  awamu ya  sita  chini  ya  Mhe  Rais Dkt    Samia  Suluhu  Hassan  kwa  kuleta  vifaa  tiba vya kisasa  na  kuboresha mazingira ya ufanyaji  kazi  hivyo wananchi  waitumie ili  kupata  huduma  bora

sauti ya Dr Mtaki akiishukuru serikali kwa kuboresha huduma za afya

Kwa  upande  wake  Mkuu wa  Wilaya  ya  Maswa   Mhe Dkt Vicent  Naano  Anney  amewataka  wananchi  wenye changamoto za  afya  wajitokeze  kwa  wingi  ili  kupata  huduma  za  kibingwa  huku akiupongeza  uongozi  wa  Halmashauri kwa  ubunifu  huo  wenye  lengo la  kusogeza  huduma  kwa  wananchi

sauti ya DC Vicent Anney akitoa wito kwa wananchi kujitokeza kupata huduma za Kibingwa
Wananchi wakiwa katika foleni ya kusubiri kupata huduma za madaktari bingwa
Daktari wa macho akimwelekeza mteja (mgonjwa ) kama anaweza kusoma maandishi kwa mbali