Sibuka FM

Dkt. Lugomela aahidi neema Maswa Mashariki

15 September 2025, 5:52 pm

Picha (mwenye kofia ni Dkt George Lugomela mgombe ubunge Jimbo la Maswa Mashariki akikabidhiwa Ilani ya ccm na Katibu wa NEC Uchumi na Fedha ndugu Joshua Mirumbe wakati wa uzinduzi wa kampeni Picha na Nicholaus Machunda

Nimekuwa serikalini kwa muda mrefu hivyo nina uzoefu wa namna ya kufuatilia na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili wananchi wa Jimbo la Maswa Mashariki, ninachoomba wanipe ridhaa ya kwenda kuwasemea huko Bungeni ” Dkt George Lugomela “

Mgombea  Ubunge  kupitia  chama cha  mapinduzi  ccm  Jimbo  la  Maswa  mashariki  lililopo Wilayani  Maswa  Mkoani  Simiyu  Dkt  George  Venance  Lugomela ameahidi kutatua  changamoto za  Maji,  Afya, Elimu na Kilimo  endapo atachaguliwa  kuwakilisha  wananchi  kwa  nafasi  ya Ubunge,

Dkt  Lugomela  amesema wakati  wa  Uzinduzi  wa  kampeni  za  uchaguzi  zilizofanyika  katika  Kijij cha  Ipililo, kata  ya  Ipililo  Wilayani  hapa  na  kusema  kuwa  kumekuwepo na  changamoto  nyingi  ambazo  ameziona  hivyo  anaomba  ridhaa  ya  Wananchi  ili akazitafutie  ufumbuzi   katika ngazi  za  juu za  maamuzi

sauti ya George Lugomela – mgombea ubunge jimbo la maswa mashariki

Aidha  Dkt  Lugomela  amesema  kuwa  Serikali  imefanya  mambo  makubwa  katika utekelezaji  wa miradi ya  maendeleo  katika   Jimbo la  Maswa  Mashariki  hivyo  ameahidi   kwenda  kuendeleza  yote yaliyoanzishwa  ili  kuleta  tija iliyokusudiwa  kwa  wananchi

sauti ya George Lugomela – mgombea ubunge jimbo la maswa mashariki
wananchi wa Ipililo waliojitokeza kushiriki uzinduzi wa kampeni za ccm Maswa mashariki

Kwa  upande  wake  Mjumbe wa  kamati  kuu ya  ccm Taifa  na  Katibu wa  NEC  Uchumi  na  Fedha   ndugu  Joshua  Chacha  Mirumbe  amewataka  wana ccm  kuvunja  makundi  na  kumnadi  mgombea  aliyepitishwa  na  chama  katika Uchaguzi wa   Rais,  Wabunge  pamoja  na  Madiwani

sauti ya katibu wa NEC uchumi na Fedha ndugu Joshua Mirumbe

Shemsa  Mohamedi   ni mwenyekiti  wa  ccm  mkoa  wa  Simiyu amewataka  wanaccm na  wananchi wa  Maswa  kuhakikisha  wanaichagua  ccm  ili  iweze kuleta  maendeleo  kwa   Wananchi  ifikapo   tarehe  29. Oktoba, 2025

sauti ya Shemsa Mohamed -mwenyekiti wa ccm mkoa wa Simiyu

Nao  baadhi ya  makada  wa  ccm,  Stanslaus  Nyongo na George  Mayunga  wakapata  nafasi  ya  kuzungumza   na  wana ccm  na  wananchi  wa  Ipililo  na  kumuombea  kura  mgombea  Ubunge  Jimbo la  Maswa  Mashariki  Dkt  George  Lugomela

sauti ya Stanslaus Nyongo na George Mayunga wakimnadi mgombea ubunge Dkt Lugomela
wananchi wakiburudika wakati wa uzinduzi wa kampeni za ccm maswa mashariki
Ndugu Joshua Mirumbe – katibu wa NEC Uchumi na Fedha
Mke wa Dkt Lugomela akimuombea kura mume wake kwa wananchi wa Ipililo