Sibuka FM

Maswa: Wajasiliamali na vikundi maalumu  wapigwa msasa mfumo wa Manunuzi-NeST

11 September 2025, 11:59 am

Washiriki wa Vikundi maalumu vya wajasiliamali wakifuatilia mafunzo ya mfumo wa manunuzi NeST kutoka kwa wakufunzi. Picha na Nicholaus Machunda

Mfumo huu wa NeST ni mzuri maana mchakato wake wa kupata mzabuni unafanyika kwa uwazi na haki hivyo niwasihi wana Maswa na vikundi vya wajasiliamali kujiunga katika mfumo huu ili waweze kunufaika na fulsa zinazotangazwa na halmashauri na taasisi zingine za manunuzi “Elnight Mmari -afisa manunuzi halmashauri ya wilaya ya Maswa “

Zaidi ya wajasiliamali  50 kutoka  vikundi mbalimbali  Wilayani Maswa  Mkoani Simiyu, wamepewa  mafunzo juu ya  matumizi ya mfumo  wa  manunuzi wa Serikali –NeST   pamoja  na  fulsa zinazopatika  katika  mfumo  huo

Akizungumzia  mfumo  huo  na  fulsa  zinazopatika,  afisa kutoka  Mamlaka ya Udhibiti wa  ununuzi wa Umma –PPRA  Bi, Glory  Didas  amesema  kuwa vikundi  vitakapojisajili  katika  mfumo  huo  watakutana  na fulsa  za  Serikali  zitakazowasaidia  kuinuka  kiuchumi  na  kuongeza  pato la  Taifa

Eveline  Kapologwe  ni  mwakilishi  kutoka  Ofisi ya  Rais  Tawala za  Mikoa  na Serikali za  Mitaa- Tamisemi  amesema  mafunzo  hayo  kwa  Makundi  maalumu ya Vijana, Wanawake,Wazee na  watu wenye  Ulemavu  yatasidia kutambua  fulsa  zinazotengwa  na  taasisi  za  manunuzi

hii hapa sauti ya Eveline Kapologwe akizungumza na washiriki wa mafunzo
Bi, Elnight Mmari afisa manunuzi halmashauri ya maswa akizungumza na washriki wa mafunzo

Kwa upande  wake  afisa  manunuzi   kutoka Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Bi,  Elnight  Mmari amesema  mfumo  huo wa  NeST   unafanyika kwa  Uwazi  na  hauna  upendeleo  wowote wala kutoa  Fedha kwa  wanaoomba  Zabuni  hivyo akatoa  wito  kwa  vikundi  vya  wajasiliamali  kujiunga  kwenye  mfumo ili waweze  kunufaika   na  fulsa zinazotolewa na Halamashauri

sauti ya afisa manunuzi halmashauri ya Wilaya ya Maswa Elnight Mmari

Baadhi  ya wanavikundi   walioshiriki  mafunzo  hayo  wameishukuru  Serikali  kwa kutoa  mafunzo  hayo  kwani  yamewaongezea  uelewa  katika  mfumo  wa  manunuzi ya  Umma   na  kutoa  wito  kwa makundi  ya Vijana  kuwa  waaminifu katika  marejesho ya  fedha  wanazokopa  ili  ziendelee  kunufaisha  vikundi  vingine

sauti ya Sitta mboje-katibu wa kikundi cha Upendo-Maswa

Mafunzo  hayo  yametolewa kwa  Wajasiliamali  na  Vikundi maalumu  kwa  kushirikiana  na Idarai ya  maendeleo ya  Jamii,  PPRA, Tamisemi  na  Tasisi ya WAJIBU

Picha za matukio katika mafunzo kwa Vikundi vya wajasiliamali kuhusu mfumo wa Ununuzi wa Umma NeST yaliyofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa