Sibuka FM

Fisi waua kondoo, mbuzi wa mwenyekiti wa kitongoji Itilima

23 August 2025, 3:37 pm

Kwenye picha ni baadhi ya Kondoo waliouwaa na Fisi pale walipovamiwa Picha na Anitha Balingilaki

“Matukio ya wanyama pori wakali kuvamia makazi ya watu na kuua mifugo kuna kila namna ya kufanya kwa mamlaka za wanyama pori ili kuleta usalama kwa wananchi na mali zao lengo ni kuondoa umasikini kwa jamii kutokana na nguvu kubwa waliyoitumia hadi kuwa na mifugo”.

Na Anitha Balingilaki 

Kundi la Fisi limevamia na kuua Kondoo 17,Mbuzi watano na wengine  kujeruhiwa nyumbani kwa mwenyekiti wa kitongoji cha Mwabasambo A kilichopo kijiji cha Gambasingu kata ya Nkoma halmashauri ya wilaya ya Itilima mkoani Simiyu.

Akizungumza na Sibuka Fm mwenyekiti wa kijiji cha Gambasingu,Buka Bulugu  anaeleza namna alivyoshiriki kuwafukuza Fisi walioua mifugo ya mwenyekiti wa kitongoji cha Mwabasambo pale walipovamia Kondoo na Mbuzi.

Hatua hiyo imekuja ikiwa zimepita siku chache tangu fisi kuua na  kushambulia kondoo na mbuzi nyumbani kwa Singisi Kija ambaye ni mwenyekiti wa kitongoji cha Mwabasambo “A”.

Sauti ya Buka Bulugu Mwenyekiti wa kijiji cha Gambasingu

Akizungumza kwa masikitiko makubwa,Singisi Kija  mwenyekiti wa kitongoji cha Mwabasambo “A”, ambaye ndiye mmiliki wa Kondoo na Mbuzi zilizouliwa na Fisi anaeleza hali ilivyokuwa na hasara aliyoipata kutokana nguvu kubwa aliyoitumia kuwekeza kwenye mifugo hiyo.

Sauti ya Singisi Kija mwenyekiti wa kitongoji cha Mwabasambo A akielezea tukio lilivyokuwa

Kwa upande wao Sitta Kija na Lucas Kikaja wakazi wa kijijini hapo wameomba mamlaka husika kuwa thibiti wanayama wakali ili wasiendelee kuleta maumivu kwa jamii.

Sauti ya mashuhuda wa tukio wakiomba mamlaka kuwathibiti wanyama wakali.

Katika hatua nyingine mwenyekiti wa kijiji cha Gambasingu,Buka Bulugu akatoa ushauri kwa jamii wa kujenga mabanda/mazizi imara ili kukabiliana na changamoto za wanyama hao.

Sauti ya Buka Bulugu mwenyekiti wa kijiji cha Gambasingu.

Mfugaji huyo kabla ya tukio alikuwa na jumla ya mbuzi na kondoo 53.