Sibuka FM

Nyumba ya milioni 73 yateketea kwa moto Maswa

21 June 2025, 5:36 pm

Kwenye picha ni muonekano wa nje wa nyumba iliyoteketea kwa moto ambayo ni mali ya Bi.Anitha mkazi wa mjini Maswa Picha na Neema Solo

Tuendelee kuwakumba wenye uhutaji katika kurudisha faraja kutokana na familia hizo kupitia kwenye changamoto kwa kipindi hicho na hii ni ibada kubwa sana kwa Mungu wetu kwa kutoa sadaka kwa wenye changamoto mbalimbali”.

Na, Daniel Manyanga 

Jamii wilayani Maswa mkoani Simiyu imekumbushwa kuzikumba familia zenye mahitaji maalum katika kurejesha furaha kutokana na changamoto mbalimbali inazopitia familia husika.

Muonekano wa picha ya pamoja ikionyesha viongozi wa Juniors and Child Care Foundation (JACCAFO) na familia iliyopata janga hilo la kuunguliwa kwa nyumba Picha na Neema Solo

Ombi hilo limetolewa na mkurugenzi wa taasisi ya Juniors and Child Care Foundation (JACCAFO), Joseph Ngeleja Jidayi wakati akitoa msaada wa mahitaji mbalimbali muhimu kwa familia ya Bi.Anitha ya mjini Maswa iliyopata janga la kuungua kwa moto nyumba ambayo wanaishi mnamo tarehe 06.06.2025 majira ya saa saba usiku huku chanzo cha moto huo kikitajwa kuwa ni hitilafu ya umeme iliyoanzia kwenye nguzo ya umeme.

Sauti ya mkurugenzi wa Juniors and Child Care Foundation(JACCAFO) , Joseph Ngeleja

Ngeleja ametoa shukrani kwa watu wote walioguswa kwa kutoa michango yao huku akitaja thamani ya vitu vyote vilivyotolewa kwenye familia hiyo.

Sauti ya mkurugenzi wa JACCAFO, Joseph Ngeleja akitoa shukrani kwa wote walioguswa na kuchangia

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa tukio la utoaji wa msaada huo katibu wa Juniors and Child Care Foundation (JACCAFO),Roseanna Sewangi amesema kuwa kama taasisi wataendelea kugusa jamii kadri ya uwezo wao ili kurejesha tabasamu kwa watu.

Sauti ya katibu wa Juniors and Child Care Foundation JACCAFO

Masule Mboje na Anitha Tinya ni wanafamilia waliopatwa na janga hilo la moto wameishukuru taasisi hiyo kwa kuwakumbuka katika kipindi hichi kigumu wanachopitia hivyo jamii iendelee kutoa msaada kutokana na wao kuhitaji msaada mkubwa kwa muda huu huku wakitaja thamani ya nyumba na vitu vilivyoteketea kwa moto ndani ya nyumba.

Sauti ya wahanga wa moto