Sibuka FM

Eguity Bank kupiga jeki ununuzi zao la pamba Maswa

18 June 2025, 9:43 pm

kwenye picha kushoto mwenye shati jeupe ni Naibu waziri Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji na (Mb)Jimbo la Maswa Mashariki Stanslaus Nyongo,akifuatiwa na Waziri wa kilimo Mh,Hussen Bashe mwenye kofia,kulia mwisho Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt,Vicent Naano Anney.Picha na Samwel Mwanga

Hamasa ya ulimaji wa zao la Pamba wilayani Maswa mkoani Simiyu huenda ukaongezeka kufuatia ongezeko la uwekezaji wa viwanda vya kuchakata na kuchambua mali ghafi ya zao la Pamba mkoani hapa.

Na,Alex Sayi          

Bank ya Eguity imejitanabahisha kufanya mapinduzi kwa kushiriki nakuchochea hamasa ya ununuzi wa zao la Pamba kwa bei yenye tija kwa wakulima wilayani Maswa mkoani Simiyu

Akizungumza na Sibuka fm wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri wa Muungano Tanzania mkoani Simiyu Meneja wa biashara toka Bank ya Equity Mwanza(CPA)Emerald Landy Mutajwaa   amesema kuwa Equity Bank wamefadhili mtaji kwa ajili ya shughuli za ununuzi wa zao la Pamba

Kwenye picha Meneja biashara Bank ya Equity Mwanza (CPA)Bi,Emerald Mutajwaa.Picha na Samwel Mwanga
Sauti ya (CPA)Bi,Mutajwaa Meneja biashara Bank ya Equity

Ham Ngaza mwananchi na mkulima mkazi wa Kijiji cha Ng’hami kata ya Nyalikungu wilayani Maswa mkoani hapa amesema kuwa ongezeko la bei linawanufaisha wakulima wa zao hilo

Sauti ya Ham Ngasa mkulima

Akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara Juni 18/2025 maeneo ya viwanja vya Nguzonane akiwa ziarani wilayani Maswa Mkoani hapa  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hasan amesema kuwa wakulima wa zao la Pamba wanapaswa kuendelea kuzalisha zao hilo kwa kuwa kwa sasa soko lipo

Sauti ya Rais Mhe,Dkt,Samia

Aidha Mhe.Dkt.Samia amempongeza mwekezaji huyo huku akiahidi kutoa ushirikiano kwa mwekezaji huyo nakumtaka mwekezaji huyo kuongeza uwekezaji

Sauti ya Rais Mhe.Dkt.Samia