Sibuka FM

Kiwanda cha Bio-sustain kuzalisha ajira zaidi ya 800 Wilayani Meatu

17 June 2025, 5:34 pm

Picha Naibu waziri wa viwanda na biashara Mh Exaud Kigahe akizungumza na waandishi

Maelekezo ya Mh Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha Wizara inatengeneza Mazingira mazuri ya Uwekezaji na ufanyaji Biashara

Imeelezwa  kuwa  zaidi  ya  ajira  350   za moja kwa moja  kwa  wazawa  na zingine  800  zisizo za  moja  kwa  moja  zitazalishwa  kutoka  kiwanda  cha  kutengeneza  na  kuchakata  pamba  cha  BIO-SUSTAIN  kilichopo  Wilayani  Meatu   Mkoani  Simiyu

Hayo  yamesemwa  na  Naibu  waziri  wa  Viwanda  na  Biashara   Mhe  Exaud  Kigahe  wakati  wa  Uzinduzi  wa  kiwanda  hiyo  na  kusema  kuwa kiwanda  hicho kitaenda  kuongeza  fedha  za  kigeni  na  uzalishaji  wa  mafuta  ya  kula  yanayotokana na  mbegu  za  pamba

sauti ya mhe Exaud Kigahe Naibu waziri wa viwanda na Biashara

Mhe   Kigahe  amesema  kuwa  mipango  ya  Serikali ni kuhakikisha   inaboresha  mazingira  ya  Ufanyaji  biashara   na  uwekezaji  kwa  wazawa  ili  kuleta  tija  kwa  Taifa  

Sauti ya Mhe Exaud Kigahe

Salum  Halfan  ni  meneja wa  kiwanda  cha   kuzalisha  pamba    amesema  uwekezaji  wa  kiwanda  hicho  ni   zaidi  ya  Bilioni  14  kikiwa  na  uwezo  wa  kuzalisha pamba mbegu na  pamba nyuzi   zaidi ya   kilo  laki  5  kwa   siku

Sauti ya Salum Halfan Meneja kiwanda

Kwa  upande   wake  Mbunge   wa  Jimbo  la  Meatu  Mhe  Leah  Komanya  amesema  uwepo  wa  kiwanda  hicho  unaenda   kuchochea  ajira  kwa  wananchi   huku  kipaombele   kikiwa  ni   wananchi   wazawa   wa  Wilaya  ya  meatu  na  Mkoa wa Simiyu

Sauti ya Leah Komanya -Mbunge wa Meatu