Sibuka FM

Dkt.Samia arejesha kicheko kwa wakulima wa pamba

17 June 2025, 8:34 am

Kwenye picha ni Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan baada ya kufungua kiwanda cha kuchambua pamba na kutengeneza mabomba ya maji Picha Nicholaus Machunda

Tunapandisha zao moja baada ya jingine niseme tu kuwa zao la pamba ni wapo ya mkakati uliyopo katika kuleta uhalisia wa gharama anazotumia mkulima ili uchumi wa mtu mmoja mmoja na mkoa wa Simiyu uweze kukua na kuongeza hali ya wakulima kupenda kilimo hicho.”

Na, Nicholaus Machunda

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt .Samia Suluhu Hassan ameahidi kupandisha hadhi zao la Pamba kwa sababu ni tegemeo kwa mkoa wa Simiyu katika kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla kupitia zao hilo ambalo ni utambulisho wa mkoa huo.

Kwenye picha ni Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa wa serikali na chama cha mapinduzi wakiwa kwenye picha ya pamoja ya ufunguzi wa kiwanda hicho Picha na Nicholaus Machunda

Mhe.Dkt.Samia amesema hayo leo wakati akizindua kiwanda vya uchakataji wa Pamba na kiwanda cha kutengeneza bomba za maji vilivyopo katika mji wa Bariadi mkoani Simiyu.
Mhe.Dkt.Samia amesema kuwa viwanda hivyo vyenye gharama ya shilingi bilioni 8 vinavyomilikiwa na kampuni ya Moli Oil Mills kampuni LTD Vitaenda kupandisha bei ya zao pamba na kuinua uchumi wa wana Simiyu.

Sauti ya Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan akielezea namna ambavyo zao la pamba linaenda kuwa mkombozi mkubwa kwenye uchumi wa mtu mmoja mmoja na mkoa wa ujumla

Aidha katika hatua nyingine Mhe.Dkt.Rais Samia amempongeza mwekezaji wa ndani katika kiwanda cha kutengeneza mabomba ya maji kwani serikali ilikuwa inatumia fedha nyingi za kigeni kuagiza mabomba nje ya nchi hivyo itapunguza gharama ya kuagiza nje.

Sauti ya Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan akitoa pongezi kwa mwekezaji wa ndani