Sibuka FM

DC Maswa  atahadharisha  Madiwani  figisu za  Ununuzi wa  Pamba

5 June 2025, 9:15 am

Picha ni Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wakiwa katika kikao cha Baraza Picha na Nicholaus Machunda

Diwani ni haki yake kufanya biashara ya Ununuzi wa Pamba kwasababu pamba siyo shughuli ya Halmashauri kwahiyo hakuna mgogoro wa kimasirahi kwa diwani kununua Pamba, Lakini sitavumilia Diwani atakayefanya hujuma katika ununuzi wa Pamba mimi Nitakuning’iniza tu “Mhe Dkt Vicent Anney -Mkuu wa Wilaya ya Maswa “

Madiwani  katika  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa   Mkoa  wa  Simiyu  wametahadharishwa kuhusu  Figisu   wanazofanya  katika  Ununuzi   wa  zao  la  Pamba  na  kusema kuwa hatawavumilia  wale  watakaofanya Ununuzi   halafu  wakafanya   udanganyifu  wa  kuibia   Wakulima

Tahadhari  hiyo  imetolewa  na   Mkuu  wa  Wilaya  hiyo  Mhe,  Dkt  Vicent   Naano  Anney   wakati  akitoa  Salamu  za  Serikali  katika  Kikao   cha  Baraza  la  Madiwani  liliofanyika   katika  Ukumbi wa  Halmashauri  hiyo   na  kusema  ni  haki  ya  Diwani  kununua  Pamba  lakini  lazima  atimize  sheria, Taratibu  na  wajibu  wa  ununuzi  wa  pamba

sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mh Vicent Naano Anney

Aidha  Dkt  Vicent   Anney  amewatahadharisha   Viongozi  wa   Amcos    wanaochezea  Mizani  kwa  lengo  la  kuwaibia  wakulima na  kusema  mizani ya  sasa  ina  Mfumo  ya  kisasa  ambayo  inamwezesha   Mkuu  wa  wilaya,  Bodi  ya  Pamba  na  Wizara  ya  Kilimo  kuona  mwenendo  wa  ununuzi   wakiwa  Ofisini  kwao

Sauti ya Mkuu wa Wilaya kuhusu wizi wa kuchezea Mizani ya pamba

Mwenyekiti  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Mhe,  Paul   Maige   ameishukuru  Serikali  kwa  kuleta  Fedha  nyingi  kwa  ajili  ya  Shughuli  za  Maendeleo  huku  akisema  Makusanyo  yameongezeka   hadi kufikia  asilimia  79  kulingana  na  Malengo  waliyojiwekea  katika  mwaka  wa  fedha 2024/2025

Sauti ya Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Paul Maige akitoa taarifa ya Makusanyo
Picha ni Mbuge wa Jimbo la Maswa Mashariki Mhe, Stanslaus Nyongo

Naye  Mbuge  wa  Jimbo  la  Maswa  Mashariki   Mhe  Stanslaus  Nyongo  kwa  niaba  ya  Wananchi  wa  Jimbo  lake  amemshukuru   Rais  Samia  kwakuleta miradi  kila   kata   na kuziomba  taasisi  ambazo zinatekeleza  miradi  ya Maendeleo kukamilisha  kwa  Wakati ili wananchi wanufaike kama ilivyokusudiwa

Sauti ya Mhe Stanslaus Nyongo – Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki

Kwa upande  wake  wenyekti  wa  Chama cha  Mapinduzi  ccm   Wilaya ya  Maswa   Ndugu   Onesmo  Makota  amesema  kuwa  tunapoelekea Uchaguzi  Mkuu  2025  tuendelee  kudumisha  Amani ili  uchaguzi  ufanyike  salama  na  kumalizika   Salama   huku  akiwataka  Viongozi  na watendaji  kuzitatua  changamoto ambazo  zitaleta  vikwazo  vya  Ushindi  wa  chama  hicho.

Sauti ya Ndugu Onesmo Makota – Mwenyekiti wa ccm wilaya ya Maswa