Sibuka FM

TAKUKURU yabaini milioni 26 kuliwa na viongozi wa AMCOS Simiyu

4 June 2025, 8:25 pm

Kwenye picha ni Peter Mkombe akizungumza na wanaushirika hawapo pichani akiwataka kuachana na rushwa wawapo kazini Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Rushwa ni adui wa haki na maendeleo lazima kwa nguvu zote viongozi waipinge rushwa maana leo utaona kuna watu wachache wasiokuwa waadilifu wanatumia turufu ya uongozi wao kupora haki za watu kujilimbikizia mali ambazo ni wizi na kuwanyima watu ambao walistahili haki zao kwa kuwa tu mkono mtupu haulambwi.”

Na, Daniel Manyanga 

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa  nchini (TAKUKURU) mkoa wa Simiyu imepokea malalamiko tisa ya vitendo vya rushwa kutoka kwenye vyama mbalimbali vya ushirika  Amcos mkoani hapo katika kipindi cha kuanzia mwezi January hadi sasa huku milioni ishirini na sita zikiliwa na viongozi wa ushirika wasiokuwa waadilifu.

Akizungumza na Sibuka Fm  mwakilishi wa kamanda wa TAKUKURU mkoani hapa, Peter Mkombe wakati akitoa elimu ya masuala ya rushwa  kwenye jukwaa la maendeleo ya ushirika mkoani hapa lililofanyika wilayani Itilima na kuongeza kuwa viongozi wachache wa ushirika wananufaika wao hivyo ni vyema wakawa waaminifu ili kuepuka kukutwa na sheria kali za uhujumu uchumi.

Sauti ya Peter Mkombe aliyemwakilisha kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Simiyu akizungumza na wanaushirika katika kumaliza rushwa

Akizungumza kwenye jukwaa hilo,Godfrey Mpepo  mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Simiyu amesema sheria za ushirika zipo vizuri sana hivyo hakuna kiongozi yeyote aliyeko juu ya sheria lazima wafanye kazi kwa kufuata miiko ya uongozi na kuzingatia viapo vyao.

Sauti ya mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Simiyu akielezea namna ambavyo ushirika inatakiwa kuwa safi katika swala la rushwa
Kwenye picha ni mrajisi msaidizi wa vyama vya ushirika mkoa wa Simiyu, Godfrey Mpepo akizungumza jambo katika kukemea rushwa kwa watumishi wa ushirika

Akimwakilisha mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Itilima ,Polycarp Ntapanya amewata viongozi wa AMCOS kusimamia na kuzingatia maadili ya kazi zao.

Sauti ya Polycarp Ntapanya akiwataka viongozi mbalimbali wa ushirika kuwa waadilifu katika sehemu zao za kazi
Kwenye picha ni mwakilishi wa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Itilima,Polycarp Ntapanya akiwataka viongozi mbalimbali wa ushirika kuwa waadilifu katika sehemu zao za kazi Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm