Sibuka FM

DC  Anney  ateta  na  Bodaboda Maswa,  asisitiza utii  wa Sheria

8 May 2025, 1:35 pm

Picha ni Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe Dkt Vicent Anney akizungumza na waendesha bodaboda Picha na Nicholaus Machunda

Niwaombe maafisa Usafirishaji muwe na tabia ya kujiwekea akiba kutokana na kipato chenu mnachopata kwani hii Kazi ya bodaboda huwezi kuifanya katika Maisha yako yote itafika wakati umri utagoma kuendesha pikipiki ” Dc Dkt Vicent Anney “

Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Mkoa  wa  Simiyu  Dkt  Vicent  Naano  Anney  amewataka  maafisa  Usafirishaji  maarufu  kwa  jina  la  Bodaboda kuhakikisha  wanatii  Sheria  za  Usalama  barabarani pamoja na kutoa   Ushirikiano  kwa Jeshi  la  Polisi  ili  kubaini   wahalifu  huku  akiwaomba  waunde  vikundi  ili  kupata  Bodaboda  za  Mkopo  unaotolewa  na  Halmashauri  kutokana  na  ukusanyaji  wa  Mapato  ya  ndani

Amesema  hayo  baada  ya  kukutana  na  Kundi  la  Vijana  hao  waliojiajiri  kupitia  shughuli  za  bodaboda  na  kusikiliza  Changamoto  wanazokutana  nazo  katika  biashara hiyo  ili  Serikali  ione  namna  ya kuweza   kuwasaidia

Sauti ya Dkt Vicent Anney Mkuu wa wilaya ya Maswa akiongea na Waendesha bodaboda

Aidha  Dkt  Anney  amewataka  waendesha  bodaboda  hao  kuwa  na  tabia  ya  kuwekeza  katika aseti mbalimbali   kutokana  na  kipato  cha  shughuli  wanazofanya  kwani  kazi  hiyo  hawawezi  kuifanya  katika  Maisha  yao  yote  kutokana  na umri  unavyoenda.

Sauti ya Dkt Vicent Anney akiwasisitiza kujiwekea akiba katika shughuli yao
Mkuu wa Wilaya akizungumza na waendesha Bodaboda Mjini Maswa

Mkuu  wa  Usalama  barabarani  Wilayani  hapa, Mkaguzi  Msaidizi  wa  Polisi  James  Nyorobi amewataka  waendesha  boda boda  kuzingatia  sheria  za  barabarani ikiwemo  kuvaa  kofia  ngumu, kubeba  mishikaki na  kuzingatia matumizi  ya  taa  za  kuongozea  magari

Sauti ya James Nyorobi Mkuu wa Usalama barabarani Wilaya ya Maswa
James Nyorobi Mkuu wa Usalama barabarani Wilayani Maswa

Nao  baadhi  ya  bodaboda  walioshiriki  kikao  hicho  cha  Mkuu  wa  Wilaya  wakapata nafasi  ya  kupaza  sauti  zao  kuhusu  Elimu ya  sheria za  barabarani  pamoja  na  matukio  ya uhalifu  na  Wizi  wa  Pikipiki  yanayoendelea  wilayani  hapa

Sauti ya baadhi ya Waendesha bodaboda Mjini Maswa wakielezea changamoto zao