Sibuka FM

Dkt  Lugomela  atembelea Miradi ya Maji  Maswa  aahidi kutuma watafiti

4 May 2025, 9:29 pm

Picha (mwenye kofia na tisheti ya Bluu) Dkt George Lugomela Mkurugenzi wa rasilimali za Maji kutoka Wizara ya Maji akipewa maelezo kuhusu ujenzi wa Bwawa la Maji katika Kata ya Lalago wilayani Maswa, Picha na Nicholaus Machunda

Ukanda huu wa Wilaya za Maswa na Meatu unachangamoto ya kuwa na Maji ya Chumvi hivyo nitatuma wataalamu waje kufanya utafiti wa namna ya kupata maji Mazuri maana kwa sasa Wizara ya Maji ina Mitambo ya kisasa “Dkt George Lugomela “

Mkurugenzi  wa  Rasilimali za  Maji  kutoka  Wizara  ya  Maji   Dkt  George  Lugomela  ameahidi  kutuma  wataalamu  kwa  ajili  ya  kuja  kufanya  utafiti  kuhusu  upatikanaji  wa  Maji  baridi  katika  maeneo  ambayo  yanachangamoto  ya  upatikanaji  wa  Maji  ya  chumvi.

Dkt  Lugomela   amesema  hayo   wakati  wa  kuhitimisha  ziara  yake  katika  Mkoa  wa  Simiyu   Wilaya  ya  Maswa  na  kusema  kuwa  Wizara  itatuma  wataalumu  pamoja  na   Mitambo  yenye  teknolojia ya  kisasa  itayosaidia  kubaina sehemu  za  Maji mazuri  yatakayosaidia  wananchi  wa  Maswa  na  Maeneo  mengine

Hii hapa ni sauti ya Dkt George Lugomela akielezea utafiti wa maji baridi

Aidha  Dkt  Lugomela   amemshukuru  Mhe  Rais  Samia   kwa  kutoa  fedha  nyingi  kwa  ajili  ya  Miradi  ya  Maji   pamoja  na  Ujenzi  wa  Mabawa   hasa  katika  Maeneo  yenye  hali  ya  Ukame  ikiwemo  Mkoa  wa  Simiyu  ili  kuondoa  changamoto ya  huduma  ya  Maji  huku  akiwahakikisha  wananchi  wote  waliotoa  maeneo  yao   kwa  ajili  ya  Ujenzi  wa  mabawa  watalipwa  fidia  zao

Sauti ya Dkt George Lugomela akiwahakikishia malipo ya Fidia za maeneo yao
muonekano wa Bwawa la lalago ambalo ni Mojawapo wa vyanzo vya Maji vilivyotembelewa na Mkurugenzi wa rasilimali za Maji Dkt George Lugomela

George  Itumbula  ni  Mhandisi  Ujenzi   bonde  la  ziwa  Victoria  amesema  kuwa  wote  waliotoa  maeneo  yao  kwa  ajili  ya  kupisha  ujenzi wa  Bwawa la Ipililo tayari  wameshalipwa  fidia  zao  isipokuwa  wachache  ambao  hawakuwepo  kwenye  utaratibu  wa  awali   na  kuahidi  kulifanyia  kazi  ili  nao  walipwe  stahiki zao.

sauti ya Mhandisi George Itambula -Mhandisi Ujenzi Bonde la ziwa Victoria

Awali  akitoa  maelezo  kwa  Mkurugenzi  wa  rasilimaji Maji  Wizara  ya  Maji  Dkt George  Lugomela , Meneja  wa  Wakala  wa  Maji na  Usafi  wa  Mazingira  vijijini –RUWASA    Wilayani  Maswa  Mhandisi  Lucas  Madaha  amesema  kuwa  kukamilika  kwa  mabawa hayo   yatasaidia  kuongeza  Upatikanaji  wa  huduma  ya  Maji  kwa  Wananchi

Mhandisi Lucas Madaha -Meneja Ruwasa Maswa

Baadhi  ya  Wananchi  kutoka  kata  ya  Ipililo  wilayani  Maswa  wameishukuru  Serikali  ya  Mhe  Dkt  Samia Suluhu  Hasan  pamoja  na  Dkt  Lugomela  kwa  kuwakumbuka  wananchi   wa  Ipililo  na  Maeneo  mengine  kwani  Maji ni  Uhai  na  yanahitaji  kila  sehemu.

sauti za baadhi ya wanachi wa Ipililo wakielezea kufaha yako kwa Serikali