Sibuka FM

Wafanyabiashara Maswa wakana kuchangishwa fedha za nyumba ya DC

1 May 2025, 5:47 pm

Kwenye picha wa pili kutoka kulia ni Mwenyekiti ya Jumuiya ya wafanyabiashara wilayani Maswa ,Winfrida Njige akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa jumuiya hiyo wakiwa kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo kuwasilisha waraka wa kukanusha Picha na Nicholaus Machunda

“Jumuiya ya wafanyabiashara(TTCIA)wilayani Maswa mkoani Simiyu wameonya nakutotaka jina lao kutumiwa na  watu kwa maslahi yao binafsi,hali inayowachonganisha wao na watendaji wa Serikali Wilayani hapo”.

Na,Alex Sayi-Maswa Simiyu

Jumuiya ya wafanyabiashara wilayani Maswa mkoani Simiyu(TTCIA) wamekanusha taarifa zilizotolewa mitandaoni kwenye tovuti ya Jamii foram April,28/2025 saa 03:56 asubuhi,wakilalamika kuchangishwa fedha kinyume cha utaratibu kwa ajili ya ukarabati wa nyumba ya mkuu wa wilaya ya Maswa aliyehamishiwa kutoka wilayani Bunda mkoani Mara.

Hayo yamebainishwa na baadhi ya wafanyabiashara hao wakiwa kwenye ofisi za Mkuu wa Wilaya hiyo wakati wakiwasilisha walaka wa kanusho lao hilo April.30 mwaka huu

Akiwasilisha waraka huo wa kanusho kwa mkuu wa wilaya hiyo,mwenyekiti wa jumuiya ya wafanyabiashara wilayani Maswa mkoani Simiyu ,Winfrida NJige amesema  kuwa taarifa zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii zikiwa na kichwa cha habari kilichosomeka”Maombi ya uchunguzi kuhusu uchangishaji fedha kinyume na taratibu kwa ajili ya ukarabati wa nyumba ya mkuu wa wilaya ya Maswa’‘ hazina  ukweli wowote.

Sauti ya mwenyekiti wa jumuiya ya wafanyabiashara akikanusha taarifa za kuchangishwa fedha za nyumba ya ukarabati

Akizungumza na Sibuka fm Boniphace Mabonesho mfanyabiashara wa duka wa bidhaa mchanganyiko wilayani hapa amesema  kuwa taarifa za kuchangishwa fedha kinyume na utaratibu kwa ajili ya ukarabati wa makazi ya mkuu wa wilaya ya Maswa hazina ukweli.

Sauti ya Boniphace Mabonesho akizungumza na waandishi wa habari juu ya uzushi wa taarifa za kuchangishwa fedha hizo

Kwa upande wake, Joseph Bujenja mfanyabiashara wa duka la vifaa vya ujenzi ambae ni mjumbe wa (TTCIA) wilayani hapa amesema kuwa taarifa zilizoenea mitandaoni juu ya wafanyabiashara kuchangishwa fedha na katibu tawala wilaya ili kufanikisha ukarabati wa nyumba ya mkuu wa wilaya ya Maswa kwake ni za uongo maana hajawahi kufikiwa na kuombwa mchango wa ukarabati wa nyumba hiyo

Sauti ya Joseph Bujenja mjumbe wa jumuiya ya wafanyabiashara wilayani hapo akielezea utaratibu wa namna ya kushirikiana na serikali kama Kuna jambo

Benjamini John mfanyabiashara wa vifaa vya ujenzi akizungumza na Sibuka fm amesema kuwa taarifa zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii ni uongo mtupu kama kuna mtu anataka kuwachafulia uhusiano wao na serikali ya wilaya hiyo basi aende kwingine lakini siyo wafanyabiashara

Sauti ya mfanyabiashara Benjamin John akikanusha taarifa hizo

Ikumbukwe kuwa sakata hili linajili kufuatia mabadiliko madoko yaliyofanywa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan  yaliyopelekea mabadirishano ya ofisi kati ya Aswege Kaminyoge aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Maswa aliyehamishiwa wilayani Bunda, akikabidhi ofisi Feb,26/2025 kwa Dkt Vicent Anney aliyekuwa mkuu wa wilaya Bunda.