Sibuka FM

Dc  Maswa  Dkt  Anney toa Maagizo mazito  kwa Wakandarasi wa Miradi ya  Maji

30 April 2025, 9:08 am

Picha ni Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt Vicent Anney ( mwenye suti ) akikagua Mradi wa Maji katika kijiji cha Buyubi wakati wa Ziara yake.

Niwaagize wakandarasi wanaotekeleza Miradi ya Maji katika Wilaya hii waongeze Kasi ili Wananchi wapate huduma ya Maji kama Serikali ilivyokusudia kusogeza huduma karibu na Wananchi Pia nitoe Onyo kwa Wananchi wanaoharibu Miundombinu ya Maji waache mara moja kwani tutawakamata na uwachukulia hatua “ DC Maswa Dkt Vicent Anney

Mkuu wa  Wilaya  ya  Maswa, Mkoani  Simiyu  Mhe  Dkt   Vicent  Naano  Anney  amewaagiza  Wakandarasi  wanaotekeleza  Miradi  ya  Maji  katika   wilaya hiyo  kuhakikisha  wanaongeza  kasi  katika   utekelezaji   wake  ili  wananchi  wapate  huduma  kama  ilivyokusudiwa

Mhe    Anney  amesema  hayo   wakati  wa  Ziara  yake   ya  Kushutukiza  katika  Miradi  mbalimbali  ya  Maji  inayotekelezwa  na  Mamlaka  ya  Maji  Safi  na  Usafi  wa  Mazingira   Mjini  Maswa (MAUWASA) huku  akitoa  Onyo  kali  kwa  baadhi  ya  Wananchi  wanaoharibu Miundombinu  ya  Maji  ikiwepo  kukata  Mabomba   na  kusababisha  adha  kwa  watumiaji  wa  huduma  hiyo

Msikilize Dc Maswa akitoa maagizo kwa wakandarasi wanaotekeleza Miradi ya Maji

Aidha  Dkt  Anney   amemshukuru  Mhe , Dkt  Samia  Suluhu  Hasan   Rais  wa Jamhuri  ya  Muungano  wa Tanzania   kwa  kutoa  fedha  nyingi  kwa  ajili  ya Utekelezaji  wa  Miradi  ya  Maji   kwa  Wananchi  wa  Mji  wa  Maswa   na  maeneo  jirani

sauti ya Dc Anney akimshukuru Rais kwa kuleta Fedha kwa ajili ya miradi ya wananchi wa Maswa
Mkuu wa Wilaya Dkt Vicent Anney (mwenye shati nyeupe ) akishuka ngazi wakati wa kukagua ujenzi wa Tanki la kuhifadhia Maji katika kijiji cha Hinduki

Leonard  Mnyeti  ni  Meneja  ufundi  wa  MAUWASA   amesema  kuwa  miradi  hiyo inaenda  kutatua  changamoto  ya  Upatikanaji  wa  Maji  katika  Mji  wa Maswa  na  Maeneo  jirani  yanayohudumiwa   na  Mamlaka  hiyo

Sauti ya Leonard Mnyeti akielezea miradi ya Maji inayotekelezwa na Mauwasa

Mnyeti amesema  kuwa kukamilika  kwa  miradi  hiyo  kutafanya huduma  ya  Maji  ipatikane  Saa  24 tofauti  na  sasa huduma  inatolewa  saa 16  huku akitoa   wito  kwa   wananchi  wanaofanya  shughuli  za  kibinadamu  katika  chanzo  hicho  cha  Maji  kuacha  mara  moja  ili  bwawa  liendelee  kuhudumia  wananchi  wetu  wa  Maswa

Sauti ya Leonard Mnyeti akielezea upatikanaji wa huduma ya Maji

Monica  Deus  Tubi  ni  Mkazi  wa  Kijiji  cha  Dodoma  kata  ya  Buchambi  Wilayani  Maswa  amesema  kuwa wanaishukuru  Serikali  kwa  kusogeza  huduma  ya  Maji safi  tofauti  na  hapo  awali   walikuwa  wakitumia  muda  mwingi  kutafuta  huduma  ya  Maji  badala  ya  kufanya   shughuli  za  kuwaletea  maendeleo

sauti ya Monica Tubi akiishukuru Serikali kwa kuwasogezea huduma ya Maji