Sibuka FM

MAUWASA yang’ara tuzo za mamlaka Tanzania bara

16 April 2025, 3:23 pm

Mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Maswa (MAUWASA) mhandisi, Nandi Mathias akizungumza na waandishi wa habari hawapo kwenye picha katika miaka minne ya Rais Mhe,Dkt.Samia Suluhu Hassan kwenye mamlaka hiyo namna ambavyo wameweza kutekeleza miradi mbalimbali ya maji

Tuna kila sababu ya kuupongeza uongozi wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe,Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa nanma ambayo umeweza kutekeleza dhana ya kumtua mama ndoo kichwani kwa vitendo na siyo kwa maneno leo hii maji safi na salama siyo swala la watu wachache kama ilivyokuwa hapo awali ama kweli mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni”.

Na, Daniel Manyanga

Imeelezwa kuwa jitihada zinazoendelea kufanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika sekta ya maji, zimesaidia kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wilayani Maswa kutoka asilimia 62.3 hadi asilimia 81 katika kipindi cha miaka minne hivyo kutekeleza dhana ya kumtua mama ndoo kichwani kwa vitendo.

Muonekano wa tenki kubwa la kuhifadhia maji linalojengwa katika kijiji cha Hinduki ili kuwasogezea wananchi huduma ya maji safi na salama Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mjini Maswa (MAUWASA), mhandisi Nandi Mathias  amesema kuwa katika miaka minne ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania,Mhe,Dkt.Samia Suluhu Hassan mamlaka hiyo imetekeleza na  inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ili kuweza kufikia lengo la kuzalisha huduma ya maji safi na salama kwa wananchi ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Sauti ya mkurugenzi mtendaji wa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira (MAUWASA) Mhandisi ,Nandi Mathias akizungumza na waandishi wa habari

Katika hatua nyingine mkurugenzi mtendaji huyo wa MAUWASA, amesema kuwa maboresho ya huduma ya maji yanayoendelea kufanywa na serikali yameisaidia mamlaka hiyo kuweza kujiendesha yenyewe ikilinganishwa na hapo awali ambapo ilikuwa inaitegemea serikali kwa asilimia kubwa kuweza kujiendesha.

Sauti ya mhandisi,Nandi Mathias akielezea namna ambavyo mamlaka hiyo inavyoweza kujiendesha na kuondokana na utegemezi kutoka serikali hapo awali.

Kwa upande wao Janeth Martine na Mathayo Faustine  wakazi wa wilaya ya Maswa wameeleza  namna ambavyo utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji unaofanywa na serikali ulivyowaondolea changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama iliyokuwa ikiwakabili kipindi cha nyuma katika maeneo yao.

Sauti ya wananchi wakielezea namna ambavyo miradi ya maji imewapunguzia adha ya maji safi na salama katika maeneo yao

Mamlaka ya maji safi na usafiri wa mazingira mjini Maswa (MAUWASA) chini ya uongozi wa mhandisi,Nandi Mathias imeweza kuibuka kidedea kwa kuwa mamlaka ya kwanza kwa bora wa kutoa huduma katika mamlaka zilizopo chini ya EWURA huku wakiwa washindi wa tatu kwa mamlaka zote zilizopo Tanzania bara