Sibuka FM

CCM Simiyu yaridhishwa na utekelezaji wa  miradi Maswa

14 April 2025, 12:56 pm

Kamati ya Siasa ya ccm Mkoa wa Simiyu ikiongozwa na Emmanuel Gungu -MNEC ( mwenye kofia nyeusi mbele) wakitoka kukagua Jengo la kichomea taka katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa Picha na Nicholaus Machunda

Katika Maeneo yote tuliyopita ya Mkoa wa Simiyu, Halmashauri ya Wilaya ya Maswa mmeitendea haki Ilani ya ccm maana Miradi yote tuliyokagua ipo vizuri, Usimamizi Mzuri wa fedha unaonekana, kwakweli DC na DED Rais hakukosea kuwaleta hapa, Hongereni sana na timu yenu yote inayowasaidia kufanikisha haya. “Emmanuel Gungu Silanga MNEC Simiyu ”

Kamati  ya  Siasa  ya  Chama  cha  Mapinduzi  (ccm ) Mkoa  wa  Simiyu  imeridhishwa  na  Utekelezaji  wa Ilani ya  ccm   na  Miradi  mbalimbali  ya  Maendeleo  katika Halmashauri  ya  Wilaya ya  Maswa

Miradi   iliyotembelewa  ni  mradi  ya  Kiwanda  cha  Chaki, Ujenzi wa  Ofisi ya  Halmashauri, Jengo  la  Mionzi  na  kichomea  taka  katika  Hospitali ya  Wilaya, Ujenzi  wa  Bweni  la  Wasichana  katika  Shule  ya  Sekondari  Salage  na  Ujenzi  wa  Jengo  la  Zahanati  katika  kijiji  cha  Mwamihanza

Wajumbe  hao   wakiongozwa  na  Emmanuel  Gungu  Silanga (MNEC) wameridhishwa  na  Usimamizi  wa  Fedha  zinazotelewa  na  Serikali  ya  Awamu  ya  sita  inayoongozwa  na  Rais   Mhe, Dkt  Samia  Suluhu  Hasani  kwa  ajili  ya  Miradi  ya  Maendeleo

sauti ya Emmanuel Gungu akizungumzia kiwanda cha chaki Maswa

Akitoa  taarifa  kwa  Wajumbe  wa  Kamati  hiyo  kwa niaba ya Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa   Maisha  Mtipa, afisa Mipango wa  Halmshauri hiyo   Ndugu  Julius  Ikongora   amesema  kuwa  Ujenzi  wa  Mradi  wa  Kiwanda  cha  chaki  na  Vifungashio umefikia  asilimia  99  ukiwa  umegarimu  kiasi  cha   zaidi  ya  shilingi  Bil  10

muonekano wa sehemu moja wapo ya kiwanda cha Uzalishaji chaki Maswa
Hii hapa sauti ya Afisa Mipango akitoa taarifa ya Ujenzi wa Kiwanda kwa Kamati ya Siasa ya Mkoa

Eva Ndegeleki na John Makongoro ni  wajumbe  wa  kamati  ya Siasa  ya  chama cha  Mapinduzi  Mkoa  wameshauri  kipaombele  cha  ajira  katika  kiwanda  cha  chaki  na  Vifunganishio  kizingatie  wazawa  wa  maeneo  husika  hasa  kwa  kazi  ambazo  hazihitaji  Ujuzi

sauti za Wajumbe wa kamati ya siasa ccm Mkoa wakishauri kuhusu ajira kwa wazawa

Paul  Jitula  ni  Mkazi  wa  Kijiji  cha  Nhami  ambapo  kiwanda  hicho  kimejengwa  ameishukuru  Serikali  kwa  Kujenga  kiwanda  katika  Maeneo  yao  kwani kitaongeza  ajira  kwa  Vijana   na  kuinua  Uchumi

sauti ya wananchi wa eneo husika wakiishukuru Serikali kwani wamepata ajira za muda Mfupi
Moja ya Miradi iliyotembelewa na kamati ya Siasa ni Bweni la wasichana katika shule ya Sekondari Salage iliyopo kata ya Nyabubinza wilayani Maswa lenye uwezo wa kubeba wanafunzi 80
Muonekano wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Maswa linalojengwa maeneo ya Nhami