Sibuka FM

Maswa: Mnadani wapanda miti kurudisha uoto wa asili

13 April 2025, 1:31 pm

Wananchi wa Kitongoji cha Mnadani kilichopo kata ya Nyalikungu Wilayani Maswa, Mkoani Simiyu wakiwa katika zoezi la kupanda Miti katika Maeneo yao. Picha na Nicholaus Machunda

Sisi wananchi wa Kitongoji cha Mnadani tumehamasika kupanda miti hasa kipindi hiki ambapo mvua zinaendelea kunyesha kwa sababu miti ina manufaa makubwa sana kwetu sisi binadamu pamoja na kulinda uoto wa asili wa ardhi yetu

Wananchi  wa  Kitongoji  cha  Mnadani  Kilichopo  kata  ya  Nyalikungu  Wilayani  Maswa Mkoani  Simiyu  wamehamasika   kupanda  Miti  katika  Maeneo  yanayozunguka  Kitongoji  hicho  ili   kurudisha  uoto  wa  Asili    na  Utunzaji  wa  Mazingira.

Wakizungumza  na  Radio  Sibuka  Fm  baadhi  ya  Wananchi  hao  wamesema  kuwa  wameamua  kuwa  na kampeni  ya  kupanda  miti  ili kuboresha  Mazingira kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho  na  kupunguza  hali  ya  Ukame

Sauti za Wananchi wa Kitongoji cha Mnadani wilayani Maswa

Wamesema  kuwa  Miti  inafaida  nyingi ikiwemo   kuleta hali  nzuri  ya  hewa,  Vivuli  majumbani, Kutengeneza Mbao, na  kurudisha uoto  wa  Asili  katika Ardhi

Sauti za Wananchi wakielezea faida za Miti

Anania  Batungi  ni  mwenyekiti  wa  Kitongoji  cha  Mnadani  amesema  wameamua  kuwa  na  kampeni  hiyo   katika  kitongoji  chake  ili   kuunga  Mkono  agizo  la  Serikali  la  kupanda  miti  hasa  kipindi  hiki  cha  Mvua   huku  akiomba  Serikali  iwape  ushirikiano inapowakamata  waharibufu  wa  Miti

Sauti ya Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mnadani akieleza kampeni ya upandaji wa Miti
Wananchi wa Mnadani wakiwa katika zoezi la Upandaji miti