Sibuka FM

Ulinzi shirikishi wapunguza vitendo vya uhalifu Simiyu

5 February 2025, 5:06 pm

Kwenye picha ni muonekano wa Insp.Francis Msuku akiwa kwenye majukumu ya kuelimisha jamii kupitia redio Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

Usalama wa raia na mali zake siyo jukumu pekee la jeshi la polisi nchini lakini tukishirikiana na jamii kwa ukaribu kupitia jeshi la jadi sungusungu tunaweza kumaliza vitendo vya kiahilifu katika maeneo yetu ya bila kutegemea hata jeshi la polisi waje watulinde ’’.

Na,Daniel Manyanga

Imeelezwa kuwa uwepo wa polisi jamii na ulinzi shirikishi katika maeneo mbalimbali  mkoani  Simiyu imesaidia kupunguza vitendo vya uhalifu na kuongeza ulinzi katika jamii tofauti na hapo mwanzoni .

Kwenye picha ni muonekano wa jeshi la jadi Sungusungu wakiwa kwenye picha ya pamoja Picha kutoka maktaba ya Sibuka fm

Hayo yamesemwa na kaimu mkuu wa  kitengo cha polisi jamii mkoa wa Simiyu Inspekta, Francis Msuku wakati akizungumza na Sibuka fm ofisini kwake na kueleza kuwa ushirikishwaji wa wananchi katika masuala ya ulinzi imesaidia kupunguza vitendo hivyo.

Sauti ya insp.Francis Msuku akielezea namna ambavyo ushiriki wa wananchi katika ulinzi na usalama ulivyopunguza vitendo vya uhalifu kwenye jamii

Nao baadhi ya wakazi wa mitaa mbalimbali mjini Bariadi wameeleza namna ambavyo polisi jamii na ulinzi shirikishi ulivyosaidia kupunguza vitendo vya kihalifu katika maeneo yao.

Sauti ya wananchi wakielezea ulinzi shirikishi unavyopambana na wahalifu