Sibuka FM

DC Maswa awaita wananchi kwenye daftari la kudumu la wapiga kura

4 September 2024, 4:08 pm

Pichani ni mkuu wa wilaya ya Maswa, Aswege Kaminyoge mwenye kaunda suti na miwani akijiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura Picha na Samwel Mwanga.

Uboreshaji wa taarifa katika daftari la kudumu la wapiga kura ni msingi mmoja wapo wa kupata viongozi bora kwa mustakabali wa Taifa letu hivyo ni muhimu kushiriki zoezi hilo.”

Na , Daniel Manyanga

Mkuu wa wilaya ya Maswa mkoani Simiyu Aswege Kaminyoge ametoa wito kwa wananchi wilayani hapo kujitokeza Katika zoezi uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura lililoanza mnamo tarehe 04 mpaka September 10 mwaka huu Ili waweze kuwa na sifa za kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu hapo mwakani.

Aswege Kaminyoge ametoa wito huo mapema leo hii alipotembelea baadhi ya vituo vinavyoandikisha kwa lengo la kujionea mwitikio wa wananchi na namna zoezi linavyoendeshwa katika halmashauri ya wilaya hiyo.

Sauti ya DC Maswa akitoa wito kwa Wananchi katika uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura
Pichani ni mkuu wa wilaya ya Maswa , Aswege Kaminyoge akipewa maelekezo kutoka kwa afisa mwandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.

Aswege Kaminyoge ameyataka makundi ambayo yatahusika katika zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura.

Sauti ya DC Maswa akitaja makundi yatakayohusika katika zoezi la uboreshaji wa taarifa

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa wilaya ametoa agizo kwa viongozi wa serikali za mitaa kutoa taarifa za vifo kwa watu ambao walioandikishwa katika daftari la kudumu la wapiga kura mwaka 2019 ili waweze kuondolewa kwa majina yao katika daftari hilo kabla ya kuingia kwenye uchaguzi mkuu na serikali za mitaa.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Maswa, Aswege Kaminyoge akitoa maagizo kwa viongozi wa serikali za mitaa.