Sibuka FM

Takukuru Simiyu  ilivyorejesha  Furaha  ya  Wananchi  Wilayani  Itilima

1 September 2024, 6:11 pm

Pichani ni Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Simiyu Aron Misanga

Na Nicholaus Machunda

Taasisi  ya  Kuzuia  na  Kupambana  na  Rushwa  Takukuru  Mkoa  wa Simiyu imefanikiwa  kurejesha  furaha  ya Wananchi  wa  Wilaya  Itilima  baada  ya   kufuatilia   Mradi  wa  Maji   katika  kijiji  cha  Ng’wang’wita  uliotoa  Huduma  ya  Maji  kwa  Mwezi  mmoja  tu  baada  ya  kukamilika

Akitoa taarifa   ya  Utendaji  kazi Robo ya  nne ya  Mwaka  2023/2024  Naibu  Mkuu  wa  Takukuru  Mkoa  wa  Simiyu     Aron  Misanga  amesema   kuwa  Takukuru  baada  ya  kubaini  Mradi  huo  kushindwa  kutoa  huduma  kama  ilivyokusudiwa  walifanya  ufuatiliaji na  kutoa  Ushauri  hatimae  Mradi  huo  wa  Maji  ulianza  kutoa  Maji

Sauti ya Naibu Mkuu wa Takukuru (M) Simiyu Aron Misanga

Katika  hatua  ya  Uchambuzi  wa  Mifumo  Takukuru  Mkoa  ilifanya  Uchambuzi  katika  Ukataji  na   Uwasilishaji  wa  Kodi  ya  Zuio (Withholding Tax ) na  kubaini  Halmashauri za  Mkoa  haliwasilishi  Kodi  ya  zuio  katika  Mamlaka  ya  Mapato  (TRA )  baada  ya  kuzikata  kutoka  kwa  Watoa  Huduma  na  Wazabuni

Sauti ya Naibu Mkuu wa Takukuru (M) Simiyu Aron Misanga

Aidha  katika Program  ya  Takukuru  RAFIKI   Naibu  Misanga  amesema  kuwa  wamefanikiwa  kufanya  Vikao 70  katika  Kata  za Bariadi, Busega, Itilima,  Maswa  na  Meatu  na  kupokea  Kero  Zaidi  ya  500 kisha  kuzitolea  Mrejesho  kwa  Wananchi

Sauti ya Naibu Mkuu wa Takukuru (M) Simiyu Aron Misanga

Takukuru  Mkoa  wa  Simiyu  imesema  kuwa   kwa  Kipindi  cha  mwezi  Julai  hadi  Septemba,  2024  itajielekeza  zaidi  katika Utoaji  wa  Elimu  juu  ya  Mapambano  dhidi  ya  Rushwa  hasa  tunapoelekea   Uboreshaji  wa  Taarifa  katika  Daftari  la  Kudumu  la  Wapiga  Kura na  Uchaguzi  wa Serikali za  Mitaa  utaofanyika  Mwishoni  wa  Mwezi  Novemba, 2024

Sauti ya Naibu Mkuu wa Takukuru (M) Simiyu Aron Misanga