Sibuka FM

Wahandzabe Meatu wanavyotumia king’amuzi cha ndege pori kuipata asali

16 August 2024, 11:33 am

PICHANI:Mhadzabe Ezekiel Salamanda akiwa Studio.Picha na Ezra John.

Wandzabe walia na Sheria za usimamizi wa wanyama pori na mapori tengefu kuwa zimechangia kuhafifisha usitawi wa jamii hizo na kusababisha hatari ya kutoweka kwa jamii hizo zinayoishi porini.

Na,Alex Sayi.

Jamii ya kihandzabe imebainisha kuwa kwa miaka nenda rudi imekuwa ikiwatumia Ndege pori kuwasaidia kubaini ilipo asali ambacho ni  ndio chakula  chao kikuu kwa jamii hiyo.

Hayo yamesemwa na Ezekieli Salamanda mkazi wa Makao Meatu Mkoani Simiyu ambae ni mhandzabe wakati akizungumza na Radio Sibuka fm,huku akibainisha kuwa wamekuwa wakiishi maisha yakutegemeana na viumbe hao.

Sauti ya Mhadzabe Ezekiel Salamanda

Salamanda ameongeza kuwa wakiwa porini hukabiliwa na hatari nyingi ikiwemo kukabiliana na majoka yenye sumu kali lakini hulazimika kupambana ili kuhakikisha wanapata kitoweo.

Sauti ya Mhandzabe Ezekiel Salamanda

Aidha kwa  upande mwingine jamii hiyo imesema kuwa mabadiriko ya tabia ya Nchi yameendelea kuwaathiri kwakuwa kwa sasa jamii hiyo inaendelea kupoteza asili yake,mira na tamaduni zake.

Sauti ya Mhandzabe Ezekiel Salamanda
PICHANI:Mhandzabe Ezekiel Salamanda.Picha na Ezra John