Sibuka FM

Mil.163.5 zatumika ujenzi bweni la wasichana Mwagala

12 August 2024, 7:02 pm

PICHANI:Aliye na Microphone ni Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu Aswege Kaminyoge,kulia kwake ni Godfrey Eliakimu Mnzava kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa.Picha na Alex Sayi

Kufuatia uwepo wa changamoto zinazowakabili watoto wa kike Nchini za kushindwa kumaliza masomo yao kutokana na umbali wa Shule Serikali imendelea na Mpango wake wa kuhakikisha inajenga mabweni kwa ajili ya kuwanusuru watoto hao wa kike.

Na,Alex Sayi.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa Godfrey Eliakimu Mnzava amezindua nakuweka jiwe la msingi kwenye Bweni la wasichana Mwagala Sekondari lililopo  Wilayani Maswa Mkoani Simiyu.

Bweni hilo lililopo  kijiji cha Mwagala Kata ya Lalago Wilayani hapa limegharimu zaidi ya Shillingi Mil,163.9 huku kukamilika kwa Bweni hilo kukitajwa kusaidia kupunguza utoro na mimba zisizotarajiwa shuleni hapo.

Sauti ya kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa Godfrey Eliakimu Mnzava.

Mkuu wa Shule hiyo Mwl,Jeremia Masolwa amesema kuwa kabla ya ujenzi wa Bweni hilo shule hiyo ilikuwa inakabiliwa na changamoto ya kukithiri kwa utoro na kukatisha masomo kwa sababu  ya umbali  wa shule hiyo.

Sauti ya Mkuu wa Sec, mwagala.

Maria Marko mwanafunzi wa kidato cha pili Shuleni hapo amesema kuwa anaishukuru Serikali kwa kuwasaidia kuwajengea Bweni hilo ambalo litawasaidia kupata muda wakupumzika na  kujisomea hali itayosaidia kuongeza ufaulu kwenye masomo yao.

Pichani:Ni mwanafunzi wa kidato cha pili Sec, ya Mwagala Mariam Marko.Picha na Alex Sayi
Sauti ya Maria Marko mwanafunzi Mwagala Sec,

Njile Ntungwa na Balinabas Masanja wazazi na wakazi wa Lalago  wamezungumzia namna Bweni litakavyo wasaidia watoto hao wa kike kuepuka na changamoto zilizokuwa zikiwakwamisha nakushindwa kumaliza masomo yao.

Sauti za wazazi Njile Ntungwa na Balnabasi Masanja.
PICHANI:Wakwanza kushoto ni Mzazi Njile Ntugwa na kulia kwake ni Balnabasi Masanja.Picha na Alex Sayi.

Aidha Aswege Kaminyoge Mkuu wa Wilaya  hiyo  akitoa taarifa ya jumla amesema kuwa miradi (7) imepitiwa na mbio za Mwenge wa Uhuru nyenye thamani ya Shillingi Bil,4.7,kati ya Miradi hiyo Mwenge umezindua miradi(2)kuweka jiwe la msingi miradi(3)kutembelea,kuona nakukagua miradi(2)