Sibuka FM

Maswa wamshukuru Rais Samia kwa mradi wa maji Zanzui

9 August 2024, 7:26 pm

Pichani wa Kwanza kushoto ni kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Godfrey Mzava akifuatiwa na Mwenyekiti wa ccm Wilaya ya Maswa Onesmo Makota, akifuatiwa na aliyeshika Maiki Mhe Mashimba Ndaki Mbuge wa Jimbo la Maswa Magharibi, kushoto kwake ni Nandi Mathias Mkurugenzi Mtendaji wa MAUWASA wakati wa Mbio za mwenge wa Uhuru

Na Nicholaus Machunda

Wananchi  wa  Vijiji  vya  Mabujiku, Malita  na  Zanzui  vilivyopo kata  ya   Zanzui, Wilayani   Maswa, Mkoani    Simiyu  wamemshukuru  Mh  Rais  Samia  Suluhu  Hasani  kwa  kutoa  Fedha  kwa  ajili  ya  Mradi  wa  maji  utakaonufaisha  Wakazi  zaidi  ya  Elfu Tisa.

Wananchi   hao  wamesema  kuwa  kukamilika  kwa  Mradi  huo  utaenda  kuondoa  adha  ya Upatikanaji  wa  maji  katika  Maeneo  hayo  licha  ya  Vijiji  hivyo  kuwa  kwenye  Chanzo  cha  Maji yanayotumika katika  Mji  wa  Maswa na  Vijiji  18  vinavyozunguka.

sauti za Wananchi wa Zanzui wakimshukuru Rais Samia kwa kuwaletea Mradi wa Maji

Akitoa  taarifa  ya  Utekelezaji  wa  Mradi  Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Mamlaka  ya   Maji na  Usafi  wa  Mazingira  Maswa ( MAUWASA ) Mhandisi   Nandi  Mathias  amesema   kuwa  Kukamilika  kwa  Madi huo  utaongeza   Upatikanaji  wa  Huduma  ya  Maji    kutoka  asilimia  78   hadi  kufikia  asilimia  95

Sauti na Eng Nandi Mathias akitoa taarifa ya Mradi kwa Kiongozi wa Mwenge

Mashimba  Ndaki  ni  Mbunge  wa  Jimbo  la  Maswa  Magharibi  ambapo Mradi  huo  unatekelezwaa amesema  kuwa  anamshukuru  Rais wa  Jamhuri  ya Muungano wa  Tanzania  Mhe  Samia Suluhu  Hasani  kwa  kutoa  fedha  nyingi  katika  Jimbo  lake  na  kutekeleza  azma   ya  kumtua  mama   ndoo  kichwani

Sauti ya Mashimba Ndaki Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi

Kwa  upande   wake  Kiongozi  wa  Mbio  za  Mwenge  wa  Uhuru  Kitaifa  mwaka  2024  Godfrey  Eliakimu  Mzava  amewapongeza  MAUWASA  kwa  kutekeleza   maono  ya   Rais  kwa  Vitendo  na  kuwataka   wananchi  wa  Wilaya  ya  Maswa  kujitokeza  kwa  Wingi kushiriki  nafasi  mbalimbali za  Uongozk  katika  Uchaguzi  wa  Serikali  za  Mitaa  utakaofanyika  mwishoni  mwa  Mwaka  huu.

Sauti ya Godfrey Mzava Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa 2024
Ujenzi wa tanki la kuhifadhia Maji ukiendelea
Mwenye wa Uhuru ukiwa Wilayani Maswa