Sibuka FM

Wananchi wilayani Meatu wachangia maji na ng’ombe

10 July 2024, 1:03 pm

Pichani ni muonekano wa mifugo wakiwa bwawani wakimywa maji picha ni kutoka maktaba ya Sibuka Fm

“Maji ni uhai kwa binadamu lakini wananchi wa wilaya ya Meatu wapo hatarini kupata magonjwa yatokanayo na kutumia maji  ya visima na mabwawa wao pamoja na mifugo ’’

Na,Daniel Manyanga

Wakazi wa kata ya Mwandoya wilayani  Meatu, mkoani Simiyu wameiomba serikali kuwasaidia kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama wanayoipitia kwa sasa ambapo wanalazimika kutumia maji ya visima na mabwawa kwa kuchangia na mifugo inayotumia maji ya bwawani hali inayohataraisha usalama wa afya zao.

Wakizungumza mbele ya mkuu wa mkoa wa Simiyu  Mhe.Kenani Kihongosi wakati wa mkutano wa hadhara  wa kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi  ambapo wananchi hao wakapaza sauti kwa mkuu wa mkoa kutokana na magumu wanayopitia ya kuchangia maji na mifugo.

Sauti ya wananchi wakiomba serikali kuweza kuboresha huduma za maji haswa vijijini

Awali kaimu meneja wa RUWASA wilaya ya Meatu mhandisi Bruno Paul amezitaja changamoto zinazosababisha huduma ya maji kutokuwa ya uhakika katika Kata ya Mwandoya.

Sauti ya meneja RUWASA wilaya ya Meatu akielezea changamoto katika maeneo

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe.Kenani Kihongosi ametoa maelekezo  kwa wakala wa maji  safi na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) wilaya ya Meatu kuongeza ufanisi na kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama ili kuepusha magonjwa yanayoweza kutokana na kutumia maji machafu.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Simiyu akitoa maelekezo kwa RUWASA ili kufikisha huduma maji safi na salama