Sibuka FM

MAUWASA yataja sababu za maji  kutokuwa angavu

28 June 2024, 10:07 pm

Muonekano wa Bwawa la New Sola likiwa limezingirwa na Magugu Maji hali inayopelekea Wananchi kutopata Maji ang’avu. Picha na Nicholaus Machunda

Kutokana na wingi wa mvua zilizonyesha kwa mwaka huu imepelekea bwawa letu la New Sola kuwa na magugumaji mengi pamoja na shughuli za kibinadamu zinazofanyika zimesababisha maji kutokuwa angavu ” Kasimu Kado “

Mamlaka  ya  Maji  na  Usafi  wa  Mazingira  Mjini   Maswa (MAUWASA ) imesema  kuwa  sababu  kubwa  ya  Maji  kutokuwa  ang’avu   ni  kutokana  na  kuwepo  kwa  MaguguMaji pamoja  shughuli  za  kibinadamu  zinazofanya  kando  ya  Bwawa  la  New  Sola  maarufu  kwa  jina la  Bwawa  la  Zanzui

Akizungumza  na  Waandishi  wa  Habari , Kaimu  Mkurugenzi  wa   MAUWASA     Kasimu   Abdallah  Kado  amesema  kuwa   Mamlaka  imeanza  Zoezi  la  kusafisha  MaguguMaji  katika  Bwawa  hilo  ili  wananchi    waendelee  kupata  Maji  Safi  na  Salama.

Sauti ya Kasimu Kado – Kaimu Mkurugenzi wa Mauwasa

Kaimu  Mkurugezi  huyo   ametoa  Wito  kwa  Wananchi   kuwa  na  Subira  wakati  zoezi  hilo  likiendelea  kufanyika  na  kusisitiza  Wananchi  wanaozunguka  Bwawa hilo kuendelea kutunza  vyanzo  vya  Maji  ili  visaidie  Vizazi  vya  Sasa   na  Vijavyo

Aidha  amewataka  Wafugaji  kutopeleka    Mifugo  yao  katika  Bwawa  na  Badala  yake  wapeleke  kwenye  Vituo  vilivyotengwa kwa ajili ya  Kunyweshea  maji  Mifugo  yao

Sauti ya Kasimu Kado Kaimu Mkurugenzi wa Mauwasa

    

Zoezi la kuondoa Magugumaji likiendelea katika Bwawa la New Sola – Maswa