Sibuka FM

Watembea umbali wa kilomita 35 kufuata huduma za TRA mjini Maswa

10 June 2024, 5:47 pm

Pichani ni katibu wa wafanyabiashara mjini Malampaka,Noel Shigolo akizungumza katika kikao cha TRA na wafanyabiashara Picha na Alex Sayi

Tunaomba sana elimu ya mlipa kodi kwa wafanyabiashara itolewe kwa upana wake na mara kwa mara ili tuweze kulipa kodi kwa hiari hali itakayoweza kujenga urafiki na TRA.”

Na, Daniel Manyanga

Wafanyabiarasha wa Mji mdogo Malampaka wilayani Maswa mkoani Simiyu waomba kusogezewa kwa huduma za mamlaka ya mapato nchini(TRA)ili kupunguza gharama za kufuata huduma za ulipaji kodi kwa hiari.

Wafanyabiashara hao  wameyasema hayo wakati wa kikao cha pamoja kilichoandaliwa na (TRA) kwa lengo la kutoa  elimu ya mlipa kodi kwa hiari kilichofanyika  ukumbi wa Ntuzu uliopo mjini Malampaka.

Akizungumza na Sibuka fm,Noel Shigolo  katibu wa umoja wa wafanya biashara mjini Malampaka amesema kuwa umbali wa ofisi za (TRA) ambao ni zaidi ya Km,35 unachangia  kuchelewa kulipa kodi kwa wakati kwa baadhi ya wafanyabiashara.

Sauti ya katibu wa wafanyabiashara mjini Malampaka

Martine Kamzora mkazi na mfanyabiashara wa Malampaka  amewashukuru maafisa wa(TRA) kwa kuona umuhimu wa kukutana na  wafanyabiashara nakuweza kusikiliza kero zao zinazowafanya kukwepa au kushindwa kulipa kodi kwa wakati.

Sauti ya wafanyabiashara wakiishukuru TRA kuwafikia katika maeneo yao

Kwa upande wake ,Issack Mathayo afisa msimamizi wa kodi wilayani hapa  amesema kuwa wamelazimika kuwafikia wafanya biashara hao nakuwapa elimu ya ulipaji kodi  hali itakayosaidia kuongeza uhiari wa wafanyabiashara hao wa kulipa kodi.

Mathayo amekili changamoto ya umbali unaochangia baadhi ya wafanyabiashara wa mji mdogo wa Malampaka kuchelewa au kushindwa kulipa kodi kwa wakati.

Sauti ya Issack Mathayo akitoa elimu ya mlipa kodi Cha hiari kwa wafanyabiashara