Sibuka FM

Maswa kuchanja ng’ombe zaidi ya laki  2

26 May 2024, 10:27 am

Pichani aliyesimama ni Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Maisha Mtipa akitoa Ufafanuzi kuhusu chanjo ya Ng’ombe katika kikao cha Baraza la Madiwani Robo ya tatu 2023/2024, Kulia kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Paul Maige. Picha Na Nicholaus Machunda

Zoezi la chanjo ya mifugo ni muhimu sana kwa wafugaji hivyo kila diwani akawe balozi kwenye eneo lake ili kuhamasisha waitikie kuchanja Mifugo yao ili kujikinga na Ugonjwa wa Mapafu “Maisha Mtipa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Maswa”

Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  mkoani  Simiyu inatarajia kuchanja ng’ombe 244, 512 ili kujikinga  na ugonjwa wa mapafu unaohatarisha afya ya mifugo hiyo.

Akitoa  taarifa  kwa  Baraza  la  Madiwani  robo  ya  tatu  ya  Mwaka  wa  Fedha  2023/ 2024  kwa  Niaba  ya  Mkurugenzi wa  Halmashauri, Mkuu  wa  Division  ya  Kilimo, Mifugo  na  Uvuvi  Wilayani  hapa    Robert  Urasa  amesema  lengo la chanjo  hiyo ni  kudhibiti  Magonjwa  ya  Mifugo

Sauti ya Robert Urasa- Daico Maswa

Sylvanus  Mipawa  ni Diwani  wa  Kata  ya  Buchambi  na  Petro  Ng’wandu  Diwani  wa  kata  ya  Mwamanenge  wamesema  zoezi  hilo  laziwa  lipewe  kipaombele   ili  kunusuru  Mifugo  ya  Wafugaji   inayokufa  kutokana  na  Ugonjwa  huo

Sauti ya Sylvanus Mpiwa na Petro Ng’wandu – Madiwani

Naye  Pili  Lameck  Ndimila   Diwani viti  maalumu  kupitia  chama  cha  Mapinduzi  ccm  amesema  kuwa  idara  ijipange   kuwashawishi  wafungaji  kuitikia  zoezi  hilo  na  siyo  kutumia  Lugha  chafu na  Vitisho   kwa  Wafungaji

Sauti ya Pili Lameck- Diwani viti Maalum

Akitoa  Ufafanuzi  wa  zoezi  hilo  baada  ya  Madiwani  kuchangia  hoja,  Mkurugenzi  Mtendaji  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa   Maisha  Mtipa  amesema  ushauri  wote  uliotolewa  na  Madiwani utazingatiwa  ili  kufanikisha  zoezi  la  Chanjo  ya  Mifugo

Sauti ya DED Maswa Maisha Mtipa

Akitoa Salamu za chama Mwenyekiti  wa  Chama  cha  Mapinduzi  Wilaya  ya  Maswa  Ndugu  Onesmo  Makota  amesema  kila  Diwani  awajibike  kwenye  Oneo  lake  ili  kuleta  Maendeleo  kwa  Wananchi  huku  akisisitiza  madiwani  kuhamasisha  Wafugaji kujitokeza katika  zoezi  la  Uchanjaji  wa  mifugo

Sauti ya Onesmo Makota – Mwenyekiti wa ccm Wilaya ya Maswa
Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa