Sibuka FM

DC Anney watumishi wa halmashauri tunzeni jengo

18 November 2025, 12:25 pm

Kwenye picha ni muonekano wa nje wa jengo jipya la makao makuu ya wilaya ya Maswa likiwa bado linaendelea kujengwa Picha kutoka maktaba ya Sibuka Fm

Uzuri wa jengo kipya la makao makuu ya halmashauri ya wilaya ya Maswa ukatoe utendaji mzuri kwa watumishi wa umma katika kuwahudumia wananchi ili kutoa tafsiri sahihi ya uzuri wa jengo na kuleta tabasamu kwa wakazi wa wilaya”.

Na,Daniel Manyanga 

Mkuu wa wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, Dkt.Vicent Naano Anney amewaomba watumishi wa umma kufanya kazi kwa bidii katika kuwahudumia wananchi wilayani hapo pamoja na kutunza jengo jipya la makao makuu ya halmashauri ya wilaya ya Maswa lililopo kijiji cha Nh’ami kata ya Nyalikungu ili liweze kudumu.

Pichani aliyesimama mwenye suti nyeusi akiwa na kipaza sauti ni mkuu wa wilaya ya Maswa, Dkt.Vicent Naano Anney akizungumza na watumishi wa halmashauri ya Maswa Picha na Samwel Mwanga

Dkt.Anney ametoa rai hiyo wakati akizungumza na watumishi hao wa halmashauri ya wilaya hiyo walipokuwa wanahamia kwenye jengo hilo hafla iliyohudhuriwa na viongozi kamati ya ulinzi na usalama wilaya,watumishi wa umma,viongozi wa chama ,viongozi wa dini na kimila.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Maswa akizungumza jambo

Mkuu huyo wa wilaya ameishauri halmashauri hiyo kutangaza uuzaji wa viwanja vilivyopo karibu na jengo hilo ili kufungua uchumi katika maeneo hayo huku viongozi wa dini wakiombwa kuhubiri amani na mshikamano.

Sauti ya Dkt.Vicent Naano Anney mkuu wa wilaya ya Maswa

Kwa upande wake afisa mipango wa halmashauri ya wilaya ya Maswa, Julius Ikongora amesema kuwa utekelezaji wa mradi wa jengo hilo ulianza mwaka 2023 na unategemea kumalizika mwishoni mwa mwaka huu huku zaidi ya billion tatu zikitumika katika ujenzi wa jengo hilo.

Sauti ya afisa mipango wilaya ya Maswa, Julius Ikongora