Sibuka FM

INEC : Tunzeni siri za  tume  msiwe  waropokaji  kwenye mitandao

28 October 2025, 11:55 am

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Maswa mashariki na Maswa magharibi Julius Ikongora wakati wa kufunga mafunzo kwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura. Picha na Nicholaus Machunda

Jiepusheni na magroup songozi ya mitandaoni ili msije mkakosea na kutuma huko taarifa pia Jiepusheni na ushabiki wa vyama vya Siasa msije mkaleta tahaluki kwani nyie mnafanya kazi kwa niaba ya Tume huru ya Taifaya Uchaguzi ”Julius Ikongora John “

Wasimamizi  na wasimamizi wasaidizi wa vituo vya kupigia  kura  katika  Jimbo la  Maswa  mashariki  na  Jimbo la  Maswa  magharibi  wameaswa  kutunza  siri  kama walivyoapa  kwa  mjibu  wa  sheria  na  kanuni za  Tume  huru ya  Taifa  ya  Uchaguzi hivyo  wajiepushe  na  magroup  songozi  ya  mitandao ya kijamii  ili kuepuka  kukosea  na  kutuma  taarifa  kwenye  magroup  hayo.

Hayo  yamesemwa  na  Msimamizi wa  Uchaguzi  Jimbo la  Maswa mashariki na  Jimbo la  Maswa Maghariki  Ndugu  Julius  Ikongora  John  wakati  wa  kufunga  mafunzo  kwa  wasimamizi na  wasimamizi  wasaidizi  wa  vituo vya  kupigia  kura

Aidha  Ndugu  Julius  Ikongora   amewataka  wasimamizi  hao  kuhakikisha   wanazingatia  muda  wa  kufungua  vituo na  kufunga  vituo, kufanya  kazi kwa  Weledi  na  Uzalendo, kufanya  kazi kwa  ushirikiano na  kuzingatia  miongozo na  kanuni za Uchaguzi.

sauti ya Julius Ikongora John akizungumza wakati wa kufunga mafunzo

Ameongeza  kuwa  wasimamizi na  wasimamizi wasaidizi  wa vituo  wanapaswa  kuwa  na  Lugha  nzuri  kwa  wapiga  kura na  kutoa  vipaumbele  kwa  makundi  maalumu  ya  Watu wenye  Ulemavu,  wazee,  wajawazito na  akina  mama  wanaonyonyesha   huku  wakijiepusha  na  ushabiki  wa  vyama  vya  siasa.

sauti ya Julius Ikongora John akizungumza wakati wa kufunga mafunzo kwa wasimamizi wa vituo vya kura

Baadhi ya  wasimamizi wa vituo vya  kupigia  kura  wamezungumza  na  sibuka  Fm  na  kueleza  watakavyoenda  kuzingatia  maelekezo yote  waliyopewa  na  Tume  ili  kuhakikisha  uchaguzi  unafanyika  kwa  haki na  usalama,  wananchi wajitokeze  kwa  wingi  kupiga  kura  kwani ni haki yao ya  msingi –  “  Kura  yako haki  yako , Jitokeze kupiga  kura”

sauti za baadhi ya wasimamizi wa vituo vya kupigia kura